
Msemaji wa serikali Isaac Mwaura amesema kuwa hakutakuwa na mswada wa fedha wa mwaka 2025.
Mwaura aliweza kukashifu na kusema kuwa mwaka huu hakutakuwa na mswada wa fedha wa mwaka 2025 alisema kuwa mwanzo wanasubiri bajeti itoke katika bunge la taifa mwisho wa mwezi huu ili waweze kuangazia makadiria ya bajeti ya shilingi trilioni 4.2.
''Ningependa kusema kwa kusisitiza kuwa mwaka huu hakutawa na mswada wa fedha mwaka 2025 tunasubiri makadirio ya majeti yatoke kwenyue bunge mwishoni mwa mwezi huu.
Ila kuna baadhi ya watu ambao wameanza kusambaza habari za uongo hizo katika mitandao wakisema kuwa serikali inapanga kutoza wananchi ushuru mwingi hao ningependa kuwatangazia kuwa hao ni maaadui wa nchi wasiotutakia mema na wanatumia mitandao ya kijamii ili kuweza kuchochea umma ambapo si vyema''. Mwaura alifafanua.
Kuhusu maswala ya usalama ambapo jengo la gorofa linatarajiwa kubomolewa kule sehemu za Mombasa Msemaji wa serikali aliweza kusisitiza akisema kuwa hiyo ilikuwa chini ya sheria na katiba ya Kenya kuwa iwapo kunapotokea swala la janga la usalama wa kitaifa hivyo huhijtaji sana kwa haraka usimamizi wa jeshi la nchi ili kuhakikisha kuwa kila kitu kinaenda sambamba.
Upange wa kilimo hasahasa upande wa ugavi na usambazaji wa mbolea kwa wakulima alisema kuwa hamna mpango wala notisi kwa kusema kuwa mbolea ambayo inatolewa na serikali inauziwa kwa gharama alieza kusema kuwa mpango huo wa mbolea ya ruzuku una utaratibu maalum serikali ilikuwa ikishirikiana na serikali za Kaunti ili kuhakikisha kuwa kilakitu kinakwenda sambamba.
Kuhusu suala la chama cha wakulima kuweza kusema kuwa wanajipanga kuweza kujiondoa katika serikali ya kenya kwanza msemaji alidokeza kwa kufafanua kwa kusema kuwa serikali ilikuwa ikidumisha uhusiano mwema kati ya wakulima na serikaili .
Alisema kuwa wakulima wa miwa waliweza kupokea bonus jambo ambalo ni la kujivunia ambapo alisema kenya ina jumla ya kampuni 16 ambapo 4 kati yazo zinamilikiwa na serikali na kama njia mojawapo kwa kuimarisha hali zao vyema serikali imeimarisha sekta hiyo ya kilimo.
Alisema kuwa Kenya ilikuwa ikisafirisha na kuuza zao la majani chai kwa mataifa ya nje kwa kiwango kikubwa akisema kuwa Kenya ilikuwa inafanya vyema katika soko la limataifa kwa viwango vyote vya mazao.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!