
Wizara ya Afya imetangaza mkurupuko wa ugonjwa wa kipindundu nchini
Ni tangazo ambalo lilitolewa mnamo Aprili 8, 2025 na wizara ya afya ambapo ilisemekana kuwa msambao huo wa maradhi ya kipindupindu yaliathiri sehemu mbalimbali za taifa.
Kipindupindu ni ugonjwa hatari ambao maambukizi yake hutokana na viini ndani ya maji vinayosababishwa na kiini kiitwacho VIBRO CHOLERA , ambapo ugonjwa huo husababishwa na mtu kula chakula kichafu ambacho kina kiini.
Dalili za maradhi haya ni kutapika , kuumwa na misuli na kupoteza maji mwilini kwa wingi ambapo hudumu kwa muda wa saa mbili na tatu.
Kulingana na taarifa ya hali ya afya imedokeza kuwa kuanzia tarehe sita Aprili ,2025 jumla ya kesi 97 ikiwemo vifo vya watu sita vilikua vimeripotiwa ambapo ni kiwango cha asilimia 6.2 ambapo kesi hizo zliliripotiwa maeneo ya Migori ,Kisumu,na Nairobi.
Katika kaunti ya Migotri kesi 53 ziliripotia kikwiemo kifo cha mtu mmoja na maeneo yalioathirika ni Suna magharibi, Suna mashariki,Kuria magaribi na Kuria mashariki.
Katika kaunti ya Kisumu kesi 32 ziliweza kuripotiawa ambapo kesi 4 za vifo ziliripotiwa na maeneo yalioathirika ni Nyando na Muhoroni.
Katika kaunti ya Nairobi kesi 12 ziliripotia kisha mtu mmoja aliweza kuaga dunia na maeneo yaliyoathirika ni Kasarami ,Embakasii mashariki, embakasi ya kati Roysambu,Kibra na Dagorreti Kusini .
Wizara ya afya inashirikiana na serikali za kaunti ili kuhakikisha kuwa inazuia msambao wa maradhi hayo.
Wizara imeanzisha mikakati ya kuhakikisha kuwa inafanya ukaguzi wa karibu sana ili kuweza kuhakikisha kuwa hamna kesi nyingi zinazoripotiwa.
Kuwapa mafunzo mafisa wa afya kwa ushikiano na maafisa wa utabibu, inawapa madktari mafunzo maalumu ya jinsi ya kukabiliana na maradhi hayo hatari.
Kwa kuhakikisha kuwa inasambaza habari kwa kutumia waendelezaji wa huduma za afya mashinani pamoja na kutumia vyombo vya habari kuweza kujiendeleza na kuzuia msambao
Umma kwa upande mwingine umeombwa kuhakikisha kuwa wanapata huduma za matibabu kwa haraka na kuhakikisha kuwa wanadumisha viwango vya usafi vya hali ya juu kwa mfano kwanzia kwa kiwango cha mtu binafsi hadi kwa jamii kwa jumla.
Kunywa maji safi na kula chakula ambacho pia ni safi na kupata matibabu ya upesi iwapo dalili hizo zitaendelela.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!