Itumbi mwanablogu

Gachagua alidai kuwa Mwanablogu Dennis Itumbi na msaidizi wa kibinafsi wa rais  bwana Farouk Kibeti ndio wanaoendesha serikali.

Gachagua alizungumza hayo alipokuwa katika mahojiano mnamo Aprili 7, 2025 alipokuwa akihadithia  utendakazi wao katika serikali.

 Gachagua alidadavua kwa kusema kuwa mara kwa mara viongozi hao walikuwa wakishiriki katika uwendeshji wa serikali katika masuala mengi.

Gachagua alisema kuwa katika mikutano mingi inayofanyika ikuluni mwanablogu Dennis Itunmbi hushinda akiwa karibu na ikulu huku akisikiliza kile ambacho huwa  kinazungumziwa.

Gachagua alisema kuwa iwapo au ahisipo kuwa mazungumzo hayo hayachukui mkondo mzuri yeye huingilia kati na kuamuru rais kuwa wakati wake ulikuwa umeisha hivyo alikuwa anahitjika katika mkutano mwingine.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

''Dennis Itumbi hushinda pale ikulu mnapokuwa na mkutano na  rais  halafu asikie mazungumzo yenu hayaleti shangwe utamuona  akimwambia  rais kuwa muda wako umeisha  unastahili kuwa na  mdahalo mwingine'' Gachagua alieleza.

Ukiona habari zozote ambazo viongozi mbalimbali huwa wanatoa katika vyombo vya  habari au kusema ni mambo ambayo huwa yameandikwa na Dennis itumbi, hata ule ujumbe ambao ulisemwa na DCI kuhusu masuala ya vurugu kanisani hiyo yote ni kazi ya Itumbi''Gachagua alisema.

''Kisha kuna huyu mwingine kwa jina Farouk Kibet yeye naye huogopewa na  kila mfanyakazi wa serikali kila maafisa wa serilkali huweza kuripoti kwake ukitaka kumwona  Rais ni  lazima Faroiuk ajuwe hata mkuu wa mawaziri MusaIia Mudavadi si kakatibu na viongozi wengine wengi huweza kujiwasilsha kwake mwanzo''.Gachagua alielezea.

''Yeye ndiye hupanga  watu kule ikulu, mimi alikuwa anataka kunipanga nikakataa nilisema la siwezi kubali kupangwa na ndio maana unaona nilionekana kama mbishi na mbaya  serikalini. '' Gachagu alifafanua.

Bwana Gachagua aliweza kuelezea mambo mengi kuhusu makosa ambayo yapo katika serikali hio ya Kenya kwanza 

Aliweza kusema kuwa kitendo cha bwana rais kumfuta kazi Moses Kuria na kuja tena kumpa kazi ya kuwa mshauri mkuu wa rais  alikisawiri kitendo hicho kama kumfukuza mchumba wako na hatimaye kuja kumchukua kama yaya tena ambapo ni madharau kwake. 

''Rais kufuta kazi Moses Kuria ya uwaziri na badala yake kumpa mtu kama Kavogo huo ni upuzi  kavogo ni mbumbumbu ilihali Kuria  ni mwerevu kupindukia. Gachagua alisema.