caption

Wizara ya usalama wa  ndani kupitia kwa idara ya magereza mnamo Aprili 7, 2025 ilitoa  tangazo rasmi  katika gareti la taifa kuhusu  nafasi za kuwaajiri maafisa  wa kuhudumu katika  magereza.

Tangazo hilo linawafahamisha umma  kuwa kutakuwa na  zoezi la kuwajiri polisi wa  kuhudumu katika  madereza ya taifa mnano tarehe 30 Aprili, 2025 na kutiwa saini na kamishina mkuu wa magereza Bwana Patrick Aranduh

Hitaji rasmi kwa kila atakayetuma ombi la  nafasi hiyo  ya ajira ni kuwa ni lazima awe na stakabadhi zifuaatazo.

Lazima muomba nafasi awe ni Mkenya na awe na kitambulisho cha  taifa vilevile asiwe amehusishwa na kesi zozote  za uhalifu.

Ni lazima awe amehitimu masomo ya sekondari akiwa na alama ya gredi ya D+ kuenda juu,awe mwenye umri wa miaka 18 hadi 28, awe na  kimo au urefu wa fiti 5 na  inchi 4 kwa  wanaume ilihali fiti 5 na inchi 2 kwa kinadada.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Vilele mwenye kutuma ombi la kazi ni  lazima awe mzima kiafya , viungo vyake vya mwili viwe sawa na awe  na akili timamu  ni lazima wenye kutuma ombi hili wawe na  uwezo mzuri wa kuona na kusikia vizuri.

Hatimaye kwa akina dada hawastahili kuwa  na ujauzito wakati wa kuchuliwa au baada na wakati wa kipindi cha mazoezi.

Kwa wale mbao watakaochukuliwa watapitia kipindi cha mazoezi ya kijeshi kwa muda wa miezi isiyopungua tisa.

Zoezi hilo litakuwa  ni la  bure hamna chochote kitakacho hitajika wala kutumika kama hongo mtu yeyete  atakayepatikana akiwa ametumia stakabadhi za masomo ambazo ni  ghushi hatachuliwa na  badala yake ataweza kushitakiwa kulingana na mijibu wa sheria na kufikishwa  mahakamani kujibu  mshitaka.

Waomba nafasi hizo watahitajika kubeba kitambulisho halisi cha  taifa, cheti cha kuzaliwa, vyeti vya shule,  namba ya cheti kutoka kwa huduma ya ukusanyaji ushuru KRA PIN.

Wito ulitolewa kwa umma   kuwa uangalifu ili  kuepuka kutapeliwa na zoezi hilo  litafanyika katika sehemu mbalimbali za  taifa zilizotajwa.

Mombasa zoezi hilo litafanyika katika gatuzi dogo la Likoni,Mombasa,Nyali,Kisauni,Changamwe na Jovmvu.

Kwale  zoezi litaendeshwa katika gatuzi dogo la Matuga,Kinango,Lungalunga,Msambweni Simbahills,Samburu miongoni mwa kaunti  zingine kama Kilifi,Tanariver,Lamu,Garissa,Wajir na Mandera.