Timu ya raga ya Kenya ya wachezaji saba kila glands ilipoteza mechi yake ya fainali ya Singapore 7s 2025, baada ya kulazwa na Fiji 21-12 katika Uwanja wa Taifa wa Singapore mnamo Jumapili. 

Shujaa hapo awali walikuwa wamejihakikishia nafasi yao ya fainali baada ya kuadhibu Uhispania 12-5 katika pambano kali la nusu fainali. 

Shujaa walianza mechi hiyo ya fainali kwa njia chanya, huku wakitia kimyani mkwaju wa penalti na kuingia muda wa mapumziko wakiwa mbele 7-0. 

Hata hivyo, wapinzani wao walijibu kwa haraka baada ya mchezo kurejea, huku Vuiviawa Naduvalo akisawazishia Fiji muda mchache baadaye.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Naduvalo alikamilisha mabao yake mawili, na kuiweka Fiji mbele 14-7. Ubabe wa Fiji ulidhihirika zaidi kadiri mechi ilivyokuwa ikiendelea, huku Alusio Vakadranu akiwazolea alama zaidi iliyowapa uongozi wa 21-7.

Juhudi nyingi za Kenya zilizaa matunda, huku William Mwanji akifunga bao na kufanya matokeo kuwa 12-21. Fiji ilishikilia ushindi huo.

Safari ya Shujaa ilianza Jumamosi, walipoichapa Ireland 17-7, kabla ya kufuatisha matokeo hayo kwa ushindi wa 10-7 dhidi ya Ufaransa hadi kileleni mwa Kundi B.

Lakini pengine mchezo wa kukumbukwa zaidi wa kikosi cha Kevin ‘Bling’ Wambua wakati wa mchuano ulikuja dhidi ya Uhispania, katika mpambano mkali wa nusu fainali siku ya Jumapili.

Jaribio la kwanza dhidi ya Wahispania lilifungwa na Patrick Odongo huku Nygel Amaitsa akifunga bao na kuwapa Shujaa uongozi wa 7-0 dakika mbili kabla.  

Tikiti ya Kenya kufuzu fainali ilithibitishwa baada ya Uhispania kumpoteza Francisco Cosculluela kupitia kadi nyekundu, huku Odongo akipata bao lake ya pili kwenye mechi hiyo. 

Uhispania walifanikiwa kupata bao la kujifariji, wakitumia makosa adimu ya Wakenya huku pambano hilo likiisha 12-5.