
Seneta wa Busia na ambaye pia ni mwanaharakati wa haki za binadamu Okiya Omtatah alidai kwa kinywa kipana kuwa Kenya ni tajiri kupindua kulingana na mgao wake wa bajeti.
Kulingana na maelezo ya bwana Okiya alisema kuwa kulingana na bajeti ambayo Kenya ilijitengea ni bajeti ya kiwango kikubwa ambacho kulingana na yeye kilikuwa kiwango ambacho kilikuwa kina mgao mkubwa sana.
Bwana Okiya Omtatah aliweza kusema kuwa wakati wa kipindi cha aliyekuwa rais Uhuru Kenyatta kulingana na ukaguzi wa hesabu za rasilimali ya taifa Kenya ilikuwa na shilingi bilioni 900 ambazo zilikuwa zimesimamia raslimali ya taifa kulingana na benki kuu ya Kenya CBK.
Bwana Omtatah alikuwa amefika Kortini kushitaki uamuzi wa aliyekuwa waziri wa fedha enzi zile Akuru Yatan kwa kuondoa msamaha (waiver) kwa shilingi bilioni 900 Korti iliweza kukubaliana na yeye kuwa Serikali iliostahili kurudishia mwananchi mlipa ushuru hela ambazo ilikuwa imejiondolea kama ulipaji ushuru.
Kulingana na maelezo ya bwana Omtatah alikuwa ameishitaki serikali kupitia benki kuu kwa kuondoa msamaha wa kulipia ushuru kwa shilingi bilioni 900.
Bwana Okiya aliweza kusema kuwa kulingana na tukio hilo ambalo Aliyekuwa waziri wa fedha Akuru Yatan katika utawala wa aliyekuwa Rais Uhuru Kenyatta waliweza kuondoa msamaha huo wa kulipa pesa kutoka kwa benki kuu ya Afrika(Commercial Bank of Africa).
Hata hivyo kulingana na matamshi ya Okiya Omtatah, aliweza kusema kuwa kiwango cha bajeti ambacho taifa la Kenya lilikuwa nacho kilikuwa kiwango kikubwa cha mgao wa bajeti ambacho hata ukiweka ujumuishaji wa mataifa ya jumuiya ya Afrika Mashariki yote Tanzania,Uganda,Rwanda na Burundi bado taifa la Kenya lina raslimali nyingi.
''Kulingana na kiwango cha mgao wa bajeti ambacho taifa la Kenya linalo kulinga na zile pesa ambazo ziko katika maliasili pekee ni shilingi bilioni 900 kiwango ambacho ni cha juu sana chenye utajiri '' Okiya alisema.
Alikuwa akizungumza katika kituo cha Spice fm alipokuwa akidadavua na kuelezea hizo takwimu zake za fedha.
Hata hivyo baaada ya kushinda kesi aliyokuwa ameiwasilisha kortini siku ya ijumaa na korti kuamuru kuwa kwa shilingi billioni 700 ambazo hazikukuwa zimelipiwwa ushuru juu kwa kuondolewa zilipaswa kulipwa kwa kuwa ni mali ya mlipa ushuru.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!