CJ Martha Koome

Jaji mkuu Martha Koome  amesisiitiza  na kutangaza  hatua mathubuti  za kupambana na ufisadi katika mahakama zote nchini.

Akitoa hutoba  yake  ya kuangazia masuala ya mahakama  na hali halisi ya huduma za mahakama, Koome alisisitiza kuwa  hamna ufisadi katika mahakama na kusema kuwa wazo kama hilo halikukuwepo miongoni mwa wafanyakazi wa mahakama wote.

''Ninataka kuangazia na kuzamia katika suala la maadili na ufisadi katika mahakama zetu  chini ya huduma ya kupambana na maadili na ufisadi EACC ambapo kuna madai mengi sana ya ufisadi katika mahakama zetu.,'Koome alisema.

''Hizi  ni tetesi ambazo hatuwezi kupuuza ni madai makubwa ambayo lazima tuangazie na tuchunguze ifaavyo.''Koome alisisitiza.

''Ningependa kutangaza na kusisitiza wazi kuwa mahakama ni mahali ambapo hamna ufisadi wowote, jinsi tujuavyo na jinsi ambavyo tunafahamu na tumelizungumzia hili katika  mihadhara mbalimbali ni kuwa  tunajua sera ya angamiza ufisadi kwa  viwango vyote katika mahakama zetu bila kuogopa wala kupendelea ili kuimarisha asasi zetu za mahakama katika viwango vyote tumezindua na kuanzisha kamati mabalimbali katika mahakama zetu kote  nchini.'' Koome alifafanua.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

'' Hizi Kamati zitakuwa na wajibu wa kuaangazia jinsi  majaji wanavyotekeleza kazi zao, kutoka kwa maawakili, waawakilishi kutoka tume  huru za kupambana na ufisadi EACC miongoni mwa  washikadau wengine.

 NI vyema zaidi kama majaji kuhakiksha  jinsi majaji wanavyojitahidi kuhakikisha kuwa wanaendasambamba na mifumo ya kisasa ya teknolojia  ambapo tumeiona jinsi  teknolojia imefanya kazi ili kuhakikisha kuwa kila kitu kinaenda sambamba.

Vileile tuliona jinsi mahakama  imekuwa ikitekeleza mambo yake kwa uzuri mwanzo kwa kuhakikisha kuwa kila jambo linakwenda sambamba ikikumbukwa jinsi utumizi wa  mitandao ulivyofanya kazi  nzuri wakati wa Covid 19''Koome alielezea.

Koome alitoa tangazo hilo la kuhakikisha kuwa anapambana na ufisadi huo na kutoa  tetesi nyingi ambazo zimekuwepo kutoka kwa umma  pamoja na mawakili waliosema  kuwa ufisadi ulikuwa umekithiri katika asasi  za mahakama ambapo kupata haki ilikuwa ni vigumu.

Mwezi uliopita rais wa mawakili nchini  LSK  Faith Odhiambo aliweza kulalamika na kutaka jaji mkuu Martha koome kuangazia hali ya ufisadi katika mahakama zetu nchini.