Aliyekuwa Gavana wa Nairobi Mike  Mbuvi Sonko amejitokeza kumsaidia Irine Wambua - mwanamke aliyepofuka jicho baada ya kushambuliwa na fisi.

Akizungumza moja kwa moja katika Runinga ya Citizen Bwana Sonko alihiadi kumsaidia bi Wambua kwa matibabu ya Jicho lake ambapo jicho lake la upande wa kushoto lilipofuka pamoja na mkono wake kuliwa.

Wambua aliathirika kwa  kulipoteza jicho lake la kushoto kutokana na uvamizi wa fisi waliotaka kumla, hio ni baada ya kutupwa nje ya Lori  alimokuwa akisafiria.

Bi wambua alisimulia kwa kusema kuwa  alikuwa amebebwa na lori ila wenye kumbeba waliazimia kumrusha nje na kumuwacha akiwa hoi.

Bi wambua alisema kuwa  baada ya kutupwa nje aliweza kupatwa na fisi barabarani usiku huo ambapo aliweza  kuliwa  na fisi  na hata kupoteza mkono wake wa kushoto vilevile.

''Nilijipata mahali ambapo kulikuwa na lori nyingi  kando yake  nilisikia mtu akiongea kikamba  nikamuona  kama mtu aliyekuwa kando nikamuona  kama mtu  ambaye angenisaidia'' .Bi wambua alielezea.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

'' Nilikuwa mahali ambapo palikuwa panaitwa Mariakani baadaye tukiendelea na safari niliona wanaume wakitoa soda aina ya Mango waliniambai ninywe nikaataa'.Maskini wa Mungu Wambua alisimulia.

'' Tukiwa  katika hali hiyo ya usafiri niliona maafisa wa polisi  nilitamani kupiga nduru ila ikashindikana hapo ndipo niliona dereva akiwa amesimama na kuanza kutoa nguo  mbele  yangu  suruali yake ikiwa imefika kwa  mabgoti nikamuuliza  mbona alikuwa  anataka kunifanyia  hivyo?''. Ireine aliendelea kuelezea masaibu  yaliyomkumba.

Kufikia pale wanaume wale  walimrusha  nje  hapo ndipo alipokutana na fisi aliyemuuma jicho pamoja na  mkono wake na  kumvuta hadi  ndani ya fensi tayari  kumuangamiza.

Hata hivyo  aliweza  kuokolewa  na maafisa  wa  polisi waliokuwa  wakipita na hatimaye  kuona mwili wa binadamu ukiwa umevutwa hivyo kuweza kusaidiwa na kupelekwa kwenye kituo cha afya  kupokea matibabu. 

Kutokana na  kisa cha Irine hapo ndipo Bwana Sonko  aliposikia  stori yake  na kuguswa na  simulizi yake hatimaya alipiga simu moja kwa moja  situdioni  na  kuahidi kujitolea kumsaidia Bi Irine ili aweze kujinasua kutoka kwa masaibu yanayomkumba.

''Irine habari yako nimesikia stori yako kwa hakika inasikitisha sana hiyo kodi ya nyumba nitalipa kwa miezi mitatu halafu kuna madaktari wako hapa lion eye plant kutoka  India hapa upper hili tutakusaidia usijali jipe moyo'' bwana Sonko alisema kwa matamshi yake mwenyewe.

Bi irine aliomba usaidizi wa kufanyiwa upasuji ili apate jicho kjingine jambao ambalio Bwana Sonko alijiokeza na kusema kuwa atamsidia kwa udi na ambari.