Michael Olunga
Nahodha wa timu ya taifa ya Kenya Harambee Stars, Michael Olunga ameteuliwa kuwa miongoni mwa wawaniaji wa tuzo ya mchezaji bora wa Afrika.

Olunga mwenye umri wa miaka 31 atawania tuzo hiyo ya mchezaji bora wa kiume akimenyana na majina tajika kwenye ulingo wa soka la Afrika.

Mshambuliaji huyo wa timu ya taifa ya Kenya na Al Duhail ya Qatar  atakuwa akiwania tuzo hii inayotamaniwa na wengi pamoja na mchezaji bora wa Afrika wa 2024, Ademola Lookman wa Nigeria, na mfungaji bora wa muda wote na nahodha wa Senegal Sadio Mané.

Mchezaji wa Liverpool na Misri Mohamed Salah ambaye ni mshindi wa tuzo hiyo mara mbili pia ameingia kwenye orodha hiyo.  Stéphane Aziz wa Burkina Faso anayechezea ligii ya Tanzania kwenye timu ya Yanga ni miongoni mwa walioorodheshwa. 

 Orodha hio iliyojaa nyota ya wachezaji bora bado inawajumuisha wachezaji maarufu  kama  Kalidou Koulibaly wa Al Hilal SFC ya ligii ya Saudi na Senegal, mlinda lango maarufu wa Manchester United na timu ya taifa ya Cameroon Andre Onana.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Wateule wengine mashuhuri ni pamoja na Achraf Hakimi wa Morocco, mchezaji wa zamani wa Manchester United Eric Bailly (Ivory Coast), kiungo wa kati wa Arsenal na mchezaji wa kimataifa wa Ghana Thomas Partey, pamoja na mwenzake Mohammed Kudus wa West Ham United.

Winga wa Manchester United Amad Diallo (Ivory Coast) pia ameingia kwenye orodha hiyo, pamoja na Franck Kessié wa taifa hilo hilo

Osimhen alishinda tuzo hiyo mnamo 2023 na anaweza kurejea kwa nyingine mnamo 2025 ikiwa ataendelea na kasi yake. Kwa sasa yuko kwa mkopo huko Galatasaray kutoka Napoli. Kama ilivyobainishwa mchango wake wa mabao umewafanya mabingwa hao wa Uturuki kufuata uhamisho wa kudumu.

Nicolus Jackson alikosolewa vikali wakati wa msimu wake wa kwanza huko Chelsea, Licha ya kuwa inje kwa muda kutokana na majeraha msimu huu ana mabao tisa na asisit 2.

sherehe za huu mwaka zitafanyika nchini Morocco.