Gavana wa Kakamega mheshimiwa Fernandes Barasa alizindua mpango wake maalum wa kugawa na kusamabaza mbolea katika kaunti Nzima.

Katika chapisho rasmi kwenye ukurasa wake  wa  X bwana Barasa  aliazimia kuwagawia wakulima mbolea pamoja na mbegu za upanzi huku mpango huo ukilenga wakulima walio na mapato ya chini na familia sizizojiweza.

Mbolea hio pamoja na mbegu za upanzi zinawa kugawiwa kwa wajane na watu walio na upungufu wa viungo vya mwili(walemavu) ili wafaidi kutoka kwa  usimamizi wa Kaunti. 

Huo mpango unalenga  kusambazwa katika  maeneo yote ya maeneobunge 12 eneo bunge la Matungu likiwa ni la kuanza kupokea mbolea hiyo ya Kaunti , mpango huo umeanzia katika eneobunge la Matungu ambapo wajane ,watu walemavu na familia sisizojiweza zimepewa kipaumbele kuweza kunufaika pakubwa katika mradi  huo wa mbolea ya bei nafuu.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Gatuzi la kakamega lina maeneobunge kumi na mawili 12, Matungu,Mumias magharibi,Mumias Mashariki,Butere, Khwisero, Shinyalu,Lurambi,Ikolomani,Likuyani,Lugari,Malava na Navakholo.

Mpango huo unajiri wakati ambpo wakulima wako mbioni kuhakikisha kuwa wanapata mboea ili kuanza shughuli ya upanzi ambapo msimu  wa unpanzi tayari umekwisha ngoa nanga. 

Hata hivyo bodi  ya nafaka na mazao nchini NCPB ilikuwa imewatangazia wakulima kuwa tayari mbolea ilikuwa kwenye maghala yake  kwa hivyo wakulma walikuwa  huru kuenda kununua mbolea huku wakiwa wanajiandaa ni kwa  ajili ya upanzi.

Hata hivyo katika bodi ya nafaka na mbolea kumeripotiwa visa vya baadhi ya madalali ambao wameripotiwa kuwa katika mstari wa mbele kununua mbolea hiyo na  kuificha ili kuwapunja wakulima kwa bei ya gharama ya juu wakati ambapo mbolea hiyo itahitajika wakati   wa upanzi.

Katika sehemu za Kitale Kaunti ya Trans Nzoa Kuliripotiwa visa vya matapeli kuchulia fursa  ya kuepo kwa mbolea na badala yake kupakia mbolea ambayo ni mchanga jambo ambalo umma ulilalamikia na kuirai serikali kuwa macho ili kuweza kuwakamata walaghai hao.

Kilimo cha mahindi kwa historia pana kimekuwa ndicho nguzo muhimu sana katika maeneo ya magharibi ya Kenya huku wakulima  wengi wakishiriki pakubwa katika kilimo hicho hivyo kuongeza kiwango cha mazao nchini ambapo kilimo ndicho uti wa mgongo wataifa.