
MWANAMUME mmoja amezua mjadala katika mitandao wa TikTok baada ya video yake akisherehekea siku ya kuzaliwa ya mbwa wake kuenea.
Katika video hiyo, jamaa huyo alipamba ukumbi wake kwa puto za rangi tofauti kumuenzi mbwa wake aliyekuwa anaongeza mwaka mwingine katika maisha yake.
Jamaa huyo pia aliongeza mvuto katika sherehe hiyo kwa kumchezea mbwa wake ala ya saxophone huku mbwa akichezesha mkia kwa ishara ya furaha.
Alikuwa na marafiki na akamwalika mpiga saxophonist kucheza muziki wa siku ya kuzaliwa kwa mbwa. Video hiyo mtandaoni inanasa mshereheshaji akiwa amependeza na nyimbo kwenye hafla hiyo.
Video hiyo ilivutia maoni kinzani, baadhi wakimpongeza kwa kumuenzi mnyama wake pendwa lakini pia wengine walionekana kutofautiana naye kwa kile walihisi ni matumizi mabaya ya pesa.
Lakini je, suala la watu kusherehekea siku za kuzaliwa kwa wanyama wao pendwa ni jambo geni?
Katika miaka ya hivi karibuni, watu wamekuwa na hulka mpya ya kuwaonyesha upendo wa kiuhakika wanyama wao pendwa, zaidi hata wanavyofanya kwa binadamu wenzao.
Mwaka 2022, mwanamume mmoja kutoka nchini Kolombia aligonga vichwa vya habari alipoamua kuwaonyesha upendo mbwa wake kwa kuwasherehekea na kuwaimbia nyimbo za heri njema za kuzaliwa.
Choko, ambaye anaishi mitaa ya Bucaramanga nchini Colombia, hana mengi lakini alitumia alichokuwa nacho kuwaandalia karamu ya siku ya kuzaliwa, kisha kurekodiwa na mpita njia.
Mnasa video huyo ambaye jina lake halikutajwa alichukua video hiyo walipogundua mapenzi ambayo Choko alishiriki na mbwa wake, Shaggy na Nena.
Walipogundua kwamba alikuwa amepatwa na matatizo makubwa na keki na mishumaa, walimrekodi akiimba furaha ya kuzaliwa kwa Shaggy na kumwonyesha upendo na uangalifu.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!