Kenya Rising Stars
Mkufunzi wa timu ya taifa ya Kenya kwa vijana wasiozidi umri wa miaka 20 Salim Babu ametangaza orodha ya wachezaji 35 watakaoshiriki kwenye dimba la Afrika, AFCON.'

Michezo hiyo ya Afrika [TotalEnergies U20 AFCON] imeratibiwa kuanza rasmi tarehe 27 April 2025.

Misri watakuwa wenyeji wa mapambano hayo baada ya kupewa kijiti na CAF siku moja tu baada ya Ivory Coast kujiondoa kwa hiari kuanda dimba hilo la Africa.

Timu ya Kenya ilipangwa kwenye kundi C, ambapo mapambano yao yatahusisha washindi wa mwisho wa michezo hiyo Senegal ambao watakua wanalitetea taji hilo kwa msimu mwingine. Mahasimu wengine kwenye kundi hilo ni Zambia na Sierra Leone.

Kikosi cha Salim Babu cha watu 35 kinaorodhesha wachezaji wafuatao.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Walinda lango: -

Bernard Jairo, Wycliford Oduor na Kevin Oduor.

Walinzi:- 

Manzur Okwaro, Joseph Bate, Jackson Sane, Amos Wanjala, Cherles Junior, Baron Ochieng, Humphrey Obino, Telena Ochieng, Rodgers Wasega.

Viungo Wakabaji:

Andereas Odhiambo, Stanley Wilison, Zech Obiero, Kevin Wangaya, Emilio Brian, Irad Mshindi, Kelly Madada, Mark Shaban, Aldrine Kibet, Humphrey Aroko, Gilbert Abala, Hassan Beja, Ezekiel Omuri, Tyron Kariuki, William Gitamu, Javan Omondi, Elly Owande, Emanuel Osoro, Jerremy Bissau.

Washambuliaji:-

Lawrence Ouma, Oliver Machaka, Henry Omolo, Luis Ingavi.