Historia ya golikipa Patrick Matasi
Mwanasoka Patrick Matasi amesimamishwa kwa muda na shirikisho la soka nchini FKF akihusishwa na upangaji wa matokeo ya mechi.

Matasi atakaa nje ya soka la kulipwa kwa muda wa siku 90 uchunguzi huo ukiendelezwa na iwapo atapatikana na hatia vikwazo zaidi vitaelekezwa kwake.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 33 ambaye kwa sasa amekua AFC Leopard amechezezea vilabu kadha ikiwa pamoja na Kakamega Home boys, Police FC, Tusker fc miongoni mwa vingine.

Mchezaji huyo ambaye ameliwakilisha taifa la Kenya mara kadha aliwahi kucheza nnje ya nchi  kati ya mwaka 2018 - 2021. Aliichezea klabu ya St George ya Ethopia.