Naibu wa Rais Profesa Kithure Kindiki alisema  kuwa serikali kwa sasa ina hela za kukamilisha miradi yote ya serikali iliyosimama tangu mwaka wa 2018 hadi 2019.

Alizungumza hayo alipokuwa katika Kaunti ya Tharaka  Nithi eneo la Mucatha mnamo Alihamisi Machi 27,  2025. Katika mazungumzo yake  aliweza kusema kuwa barabara husaidia sana kusafirisha bidhaa hadi kwenye masoko mbalimbali.

Barabara zinapokuwa sawa huweza kusababisha maisha ya Wananchi kuwa bora na mufti kabisa hivyo kuendeleza uchumi wa taifa.

'' Serikali kwa sasa ina malighafi ya kutosha ya kuweza kufufua na kukamilisha miradi yote ya serikali  ambayo ilikuwa  imekwama tangu mwaka wa 2018 hadi mwaka wa 2019 kabla ya kuanza kujenga barabara zingine'' Kindiki alisema.

Akiwa  katika msafara huo aliweza kusimama katika soko la Mucatha Chuka eneo la Igamba Ng'ombe katika Kaunti ya Tharaka Nithi ili kuweza kuangalia jinsi utaratibu na mwendelezo wa ujenzi wa barabara ulivyokuwa ukiendelea wa kilomita 30 katika barabara  ya Kibugua-Itugururu -Ishiara .

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Mbunge wa eneo bunge  la  Igamba Ng'ombe bwana Patrick Munene alikuwepo katka msafara  huo  akiandamana na wananchi wa eneobunge hilo kwenye hafla hio ya  kuendeleza maendeleo mashinani.

Shughuli hio inapoendelea Rais William Ruto anatarajiwa kuruzu katika eneo pana  la Mlima Kenya  kwa hafla  ya ziara ya kuzindua miradi mbalimbali katika eneo hilo.

Hata hivyo watu wengi wanasubiri kushuhudia kuona  jinsi rais atakavyokaribishwwa katika eneo zima la Mlima  Kenya  ambalo  limei bukia kuwa ngome hasimu kwake licha ya kupata kura  nyingi  eneo hilo .

Rais William Ruto amekuwa akiwatema  viongozi kutoka eneo hilo na ambao wana ushawishi mkubwa na ambao  wawiliweza kumsaidia kujinyakulia ushindi karika uchaguzi  mkuu wa mwaka wa 2022.

Aliyekuwa naibu wa  rais  enzi zile Rigathi Gachagua aliweza kubanduliwa mamlakani na mabunge  yote mawili mwaka jana huku akisalia kuwa kijana wa mtaani kule  Mlima Kenya huku KITHURE KINDIKI  akichukua nafasi yake.

Kiongozi wa  hivi karibuni aliyeweza kutemwa na  rais kutoka  eneo hilo la Mlima Kenya ni aliyekuwa waziri wa utumishi waa Umma bwana Justine Muturi ambapo nafasi yake iliweza kuchukuliwa na mbunge wa mbeere Geoffrey Kiringa Ruku.