Komora Mubadi Jilo
 Jamaa aliyekuwa akisubiri kuhojiwa kwa wadhiwa wa mwenyekiti wa tume ya huduma kwa polisi (NPSC) alianguka na kufariki siku ya Jumanne. 

Komora Mubadi Jilo alianguka wakati akisubiri kuhojiwa na jopo jijini Nairobi, maafisa walisema.

Alikuwa miongoni mwa wagombea wanne waliotarajiwa kuhojiwa na Jopo la Uchaguzi kwa wateule wa NPSC alipoanguka katika ofisi za Tume ya Utumishi wa Umma kando ya Harambee Avenue.

Sababu ya kifo chake  bado hakijajulikani, na tukio hilo lilivuruga mahojiano kwa muda mfupi Jumanne, Machi 25. Mwili ulihamishiwa kwenye chumba cha kuhifadhia maiti wakisubiri uchunguzi wa maiti.

Komora ambaye aliwahi kugombea nafasi ya kuwa Mbunge wa Garsen bila mafanikio mnamo 2022 kwa tikiti ya PAA. Marafiki zake walimtaja kama mtu aliyekuwa akifanya kazi kwa bidii. 

Jopo lilikuwa tayari limezindua orodha ya mwisho ya wagombea wa nafasi za mwenyekiti na wanachama.

Miongoni mwao ni aliyekuwa Naibu Gavana wa Busia Kizito Wangalwa, kamishna wa zamani wa IEBC Margaret Mwachanya, mwanachama wa zamani wa IPOA Doreen Nkatha, aliyekuwa PS Micah Powon, na mbunge wa zamani Humphrey Kimani. Wengine ni pamoja na John Mutegi, Komora, Susan Oyatsi, na John Otieno.

Mahojiano ya wiki nzima yalianza Machi 24, na yale ya mwenyekiti yalihitimishwa Jumanne.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Wagombea wa nafasi hiyo ni pamoja na msemaji wa zamani wa polisi Eric Kiraithe, aliyekuwa PS Colleta Suda, bosi wa zamani wa trafiki wa Nairobi Michael Barasa, kamanda wa zamani wa polisi wa Bomet Esther Seroney, aliyekuwa DG wa NYS Matilda Sakwa, na Mkurugenzi wa NPS wa Masuala ya Jinsia na Watoto Jostice Barmao.

Wengine walikuwa Peris Muthoni, Rose Mumbua, Areba Omwoyo, Adan Abdullahi, Isaac Ole Shaasha, na Patrick Wakaba.

Tume inayomaliza muda wake, iliyoteuliwa mnamo Machi 2019, ikitumikia muhula wa miaka sita. Wajumbe wanaoondoka ni pamoja na Mwenyekiti Eliud Kinuthia, Makamu Mwenyekiti Dk. Alice Otwala, na makamishna John Ole Moyaki, Eusebius Laibuta, Lilian Kiamba, na Edwin Cheluget.

Wagombea walitakiwa kutoa vibali kutoka kwa Mamlaka ya Mapato ya Kenya, Tume ya Maadili na Kupambana na ufisadi, Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu 'HELB, Ofisi ya Marejeleo ya Mikopo Iliyosajiliwa, na Kurugenzi ya Upelelezi wa Jinai.