Charles Nyachae, mwaniaji wa nafasi ya uwenyekiti wa IEBC, mnamo siku ya Jumatatu Machi 24,2025 alisimulia jinsi alivyoonywa na watu mbalimbali wakiwemo jamaa na marafiki dhidi ya kutuma barua ya maombi ya nafasi ya uwenyekiti wa IEBC.

Alipojiwasilisha mbele ya jopo la uteuzi, Nyachae aliambia jopo kuwa watu wengi walimpigia simu kumuuliza ikiwa alikuwa tayari kufa iwapo angechaguliwa kama mwenyekiti wa IEBC na kumrithi mwendazake Wafula Chebukati.

Kulingana na usemi wa bwana Nyachae alisema kuwa hata watu wake wa karibu walikuwa wakimuonya dhidi ya kukubali kutuma maombi kwa nafasi hiyo, kulingana naye aliweza kujibu kwa kusema kuwa hakuwa tayari kufa wala kupoteza maadili akihudumu katika nafasi hiyo.

Hatimaye Nyachae aliendelea kujipigia upato kwa kujiiaminisha mbele ya jopo kuwa alikuwa muwaniaji bora zaidi kwa kuelezea yale ambayo alitekeleza kabla.

‘’Mimi na wenzangu wengine wanane tulifanya kazi kama wanachama wa jopo lililounda katiba ya Kenya ya mwaka wa 2010, azma ambayo iliweza kufanikisha kila jambo kwa uzuri zaidi.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Nilipata fursa ya kufanya kazi na mtaalamu Daktari Koki Muli kuhusu masuala ya uchaguzi ambapo niliweza kufaidi pakubwa kwa kujizolea tajiriba pana’’Nyachae alieleza.

Aliendelea kwa kusema kuwa iwapo atachaguliwa na jopo kama mwenyekiti wa tume atahakikisha kuwa  anafanya kazi kwa ushirikiano na makamishina wengine kwa ushirikiano wa karibu na kuhakikisha kuwa  anasikiliza maoni na mahitaji ya kila mshikadau katika tume nzima.

Vilevile Nyachae aliweza kuelezea juhudi za kuhakikisha kuwa suala la thuthi mbili katika uongozi linapewa kipaumbele  kwa kuzingatia kuwa ni moja ya hitaji kuu la Katiba na vyema zaidi ikiwa litafanikishwa.

Nyachae  aliweza kujieleza kwa kusema kuwa kasumba ambayo imekuwepo ya  muda mrefu kutoka kwa wakenya ya  kutoamini Tume ya IEBC ni wakati sasa lazima mifumo ya kisheria iimarihwe na kuwe na uwazi kwa kila kitu kwanzia kwa uteuzi wa mwenyekiti hadi siku ya kutangaza kwa matokeo ya  uchaguzi.

Nyachae aliweza kusema kuwa ni fikra kuu ambazo zimekuwa zimejikita  na kukolea miongoni mwa wakenya kwa kukosa Imani na tume ya uchaguzi ila akasema yeye ni sehemu ya suluhisho iwapo atachaguliwa na jopo kwa kuangazia uchapakzi wake wa hapo mbeleni.