Katikati ya mwezi huu Taifa la Kenya liliripoti kuhusu mkurupuko wa ugonjwa wa Kala -azar katika Kaunti ya Wajir.

Ugonjwa huo uliweza kusababisha vifo vya watu 18 na kuathiri zaidi ya watu 500 katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita.

Kala-azar ambao pia hujulikana kwa kimombo kama Leishmania Parasite ni ugonjwa ambao huambukizwa na aina ya kimelea kwa jina mchwakichuguu  na ambapo dalili zake ni kupoteza uzani na kuongezeka kwa maini ya binadamu.

Zaidi ya kesi 532 ziliripotiwa huku wagonjwa mbalimbali wakipona baada ya kutibiwa .

‘’Tunapambana na mkurupuko wa ugonjwa kwa hivyo tunaomba wananchi waweze kupokea matibabu kwa haraka kuzuia  vifo’’. Daktari Ali Kutoka hospitali kuu ya rufaa ya Wajir alisema.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Kulingana na dalili za shirika la afya Duniani WHO lilisema aina hio ya ugonjwa wa Leishmaniasis huweza kusababishwa na aina ya vimelea zaidi ya 20 na zaidi ya mchwakichuguu 90 huweza kusambaza ugonjwa huo.

Ilisemekana kuwa ugonjwa aina ya Kala-azar ni ugonjwa hatari ambapo ukiwachwa unaweza kusababisha vifo na kuleta madhara makubwa , ikisemekana kuwa zaidi ya jumla ya kesi asilimia  95  hazijatibiwa wala kushughulikiwa.

 Visceral Leishmaniasis-Ugonjwa huo mara nyingi umeripotiwa katika nchi ya Brazil,Afrika Mashariki na sehemu za India ikikadiriwa kwa jumla ya kesi 50,000 hadi 90,000  kulingana na kesi ambazo zimeripotiwa katika deta  za WHO.

Cutaneous Leishmaniasis- ni aina ya pili ya dalili za ugonjwa wa Kanal-azar ni ugonjwa ambao huenea sana na husababisha mchibuko wa Ngozi  na ugonjwa wa vidonda vya tumbo na kuwashwa kwa sehemu za mwili kwa ukali zaidi,  sampuli ya ugonjwa huo hutokea sehemu za Marekani, mto meditereniani na katika nchi za  milki za kiarabu. Ambpo zaidi ya Kesi 600,000  hadi milioni moja huweza kushuhudiwa.

Leishmamia parasites- ni aina ya maradhi ambayo husambazwa kutokana na kuumwa na aina ya mchwakichuguu aina ya kike ambaye hufyonza  damu ili kutaga mayai  ambapo katika kitovu chake cha kufyonza damu ni asilimia 70 ya damu za Wanyama ikiwwemo damu ya binadamu.