Aliyekuwa Mbunge wa Kisumu Magharibi Kenn Nyagudi ameaga dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu. Kifo chake kimethibitishwa na spika wa bunge la kitaifa Moses Wetang'ula.

 Spika Wetangula alithibitisha kifo cha mwanasiasa huyo kupitia ukurasa wake rasmi ya X mnamo jana Jumapili, Machi 24.

Kulingana na spika, Nyagudi ambaye ni mbunge wa zamani aliaga dunia siku ya Jumapili alipokuwa akipokea matibabu katika  Hospitali ya Kitaifa ya Kenyatta.

"Ninatuma rambirambi zangu za dhati kwa familia ya aliyekuwa Mbunge wa Kisumu Mjini Magharibi Kasisi Kenn Nyagudi. Nilipata fursa ya kutangamana naye nilipokuwa Waziri wa Masuala ya Kigeni .Aliaga dunia jioni ya leo alipokuwa akitibiwa katika Hospitali ya Kitaifa ya Kenyatta. Familia yake ifarijiwe na kupata faraja katika mikono ya Bwana," aliandikika sipika huyo ambaye pi9a ni kiongozi wa chama cha Ford Kenya.

Mbunge huyo wa zamani alichaguliwa kwa mara ya kwanza mwaka wa 2004 wakati wa uchaguzi mdogo kufuatia kifo cha Joab Omino mnamo Januari mwaka huo huo.

Mbunge huyo alihudumu kwa miaka minne hadi alipopoteza kiti hicho wakati wa uchaguzi wa 2007 kwa Olago Aluoch.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Katika uchaguzi wa 2013, baada ya kupitishwa kwa Katiba 2010, Nyagudi aligombea kiti cha Mbunge wa Kisumu ya Kati lakini akashindwa na mgombea mpya wa kisiasa Ken Obura.

Pia aliwahi kuwa mkurugenzi wa uchangishaji fedha kwa njia ya kielektroniki na uhamasishaji wa rasilimali kwa Chama cha ODM.

Aliyekuwa Waziri Mkuu Raila Odinga alimteua katika wadhifa huu mwaka wa 2016 chama hicho kikijiandaa kwa uchaguzi wa 2017. Jukumu lake lilikuwa kufikia kutafuta fedha kutoka kwa Wakenya ndani na nje ya nchi ili kusaidia katika kampeni.