
CHELSEA italazimika kupima iwapo watamsajili au laa Jadon Sancho - lakini watalazimika kutoa kiasi kikubwa cha pesa kwa Manchester United hata kama wataachana na wajibu wao wa kumsajili winga huyo kwa mkataba wa muda mrefu.
Sancho, 24, alifukuzwa na meneja wa zamani wa Mashetani Wekundu Erik ten Hag kabla ya kujiunga na The Blues kwa mkopo msimu wa joto.
Mkataba huo ulijumuisha makubaliano ambayo yatamfanya Sancho kuwa mchezaji wa kudumu wa Chelsea kwa pauni milioni 25, hata hivyo, uvumi kwamba Washikaji hao wa London wanaweza kughairi mkataba huo umeenea katika wiki za hivi karibuni.
Mazungumzo kama haya yaliambatana na msururu tasa kwa nyota wa zamani wa Borussia Dortmund, ambaye alitoa pasi tatu za mabao katika mechi zake tatu za kwanza akiwa na jezi ya Chelsea. Ameshindwa kusajili mchango wa bao moja katika miezi miwili iliyopita, ingawa.
Chelsea walifanya mazungumzo kuhusu kipengele ambacho kingewaruhusu kuachana na kukamilisha mkataba wa kudumu kwa Sancho, ingawa kwa bei.
Na kama ilivyofichuliwa kwa mara ya kwanza na The Athletic, watatozwa ada ya faini ya pauni milioni 5 – sawa na shilingi za Kenya 837,805,000 iwapo wataamua kumrudisha Sancho Manchester United.
Ingawa kumekuwa na mabadiliko ya usimamizi katika klabu ya Old Trafford tangu Sancho alipohamia London, bado haijafahamika iwapo atapewa nafasi ya kuokoa maisha yake katika klabu hiyo na Ruben Amorim.
Bila kujali kama Sancho ana mustakabali ndani ya Manchester United, beki wa zamani wa Chelsea William Gallas anasisitiza kwamba hakuna njia ya kusalia Stamford Bridge.
Aliiambia Stadium Astro: "Yeye ni mchezaji mwenye kipaji, kila mtu anajua hili, lakini hatujui kwa nini hawezi kucheza na hawezi kuonyesha kile anachoweza kufanya.”
"Akiwa Dortmund, alikuwa mzuri. Akiwa Manchester United haikufanya kazi vizuri. Alikuja Chelsea na mwanzoni tulimwona Sancho kutoka Dortmund, lakini akatoweka.”
"Sijui tatizo ni nini, lakini kwa sasa hawezi kubaki Chelsea kwa sababu anatakiwa kufanya zaidi. Unapocheza kwenye Premier League lazima ucheze kila mchezo katika kiwango cha juu zaidi. Siyo rahisi, lakini huwezi kucheza vizuri kwa mechi chache tu halafu ukatulia."
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!