Wizara ya kilimo yatarajiwa kuanza usambasaji wa magunia ya mbolea zaidi ya milioni moja kwanzia leo  24 Machi,2025.

Kulingana na taarifa rasmi  kutoka kwa Waziri wa Kilimo Mutahi Kagwe aliweza kufafanua kwa kusema kuwa changamoto ambazo zilikuwepo katika idara hiyo siku za hivi karibuni zilikuwa zimetatuliwa na hivyo  muda mwafaka wa  usambazaji wa mbolea ulikuwa umewadia.

‘’Ningependa kuwahakikishia wakulima kuwa changamoto zote ambazo zilikuwa zimeikumba wizara ya kilimo tayari zimetatuliwa na kwa hivyo kuanzia Jumatatu ya 24 Machi,2025 usambazaji wa mbolea utang’oa nanga bila matatizo yoyote’’. Waziri alisema.

Kulingana na barua iliyoandikwa na wizara hiyo mnamo Machi 22,2025 iliweza pia kudadavua na kusisitiza kwa kina umuhimu wa kilimo pamoja na wakulima kuweza kupata mbolea ili kuhakikisha kuwa  wanaimarisha kilimo katika taifa letu ili kuongeza mjazo  wa  chakula kingi nchini.

‘’Wizara ya kilimo na  mifugo ina furaha kusema kuwa kulingana na historia kubwa ambayo imekuwepo katika wizara ya kilimo kwa wakulima kupokea mbolea ambayo ina ruzuku  kwa wakulima ambao walijisaji katika  bodi ya wakulima wa kenya na udhibiti wa usimamaizi wa kimawasiliano(Kenya integrated Agricultura lManagement information  system KIAMSI) kwa ajili ya mvua nyingi watafaidi kwa sababu ya kuweza kuzalisha chakula kingi hivyo kuliepusha taifa dhidi ya kuagiza chakula nje.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Wizara hiyo pia iliweza kuelezea kuwa kwa muda bodii ya nafaka na mazao nchini(NCPB) ilihifadhi magunia ya mbolea  zaidi ya 2.6m tangu Disemba 2024 na zaidi ya mgunia 2.6 m yamesambazwa kwa ajili ya upanzi katika mvua za msimu mrefu.

Wizara pia iliweza kufafanua kwa kusema kuwa kutokana na hamu kuu na hitaji la wakulima kutaka mbolea kwa wingi hio ni kuonyesha kuwa kama taifa tutakuwa katika nafsi nzuri ya kujikimu katika kilimo siku za hivi karibuni.

Hata hivyo wizara pia ilisikitikia hali ya wakulima kufika katika bodi ya nafaka na mazao kwa ajili ya kupokea mbolea  yao ya ruzuku ila kulingana  na hitilafu za kimitambo zoezi hilo halikufanikishwa jinsi ilivyokusudiwa.

Serikali kupitia kwa Wizara hiyo ya kilmo na mifugo iliweza kusema kuwa wanafanya jitihada na juhudi zote zimewekwa ili kuhakikisha kuwa  kila kitu kinaendeshwa jinsi kilivyoratibiwa.

Wizara iliweza kutangaza kwa kusema kuwa zaidi ya magunia milioni moja yatatolewa kwa  wakulima katika matawi yote ya bodi  ya nafaka na mifugo ilioidhinishwa na kuwarai wakulima kuwa waangalifu kutokana na matapeli wanaouza mbolea ghushi ambayo haijafikia viwango vinavyohitajika,wiraza ikisema kuwa iko macho kuwaadhibisha matapeli hao kwa kuwachukulia hatua  kali za kisheria dhidi ya kumdhulumu mkulima.