Dereva Elfin Evans mwenye umri wa miaka 36 na dereva mwenzake Scott Martin ndio washindi wa toleo la 2025 la Mashindano ya Dunia ya Mbio za Magari, Safari Rally.

Timu ya Toyota Gazoo ilifunga mchuano huo kwa kuendeleza uongozi hadi pointi 36 baada ya raundi tatu.

Akizungumza baada ya ushindi huo, Evans alisema ni ushindi mkubwa kwa timu hiyo, kwani ndiyo wameifanyia kazi.

"Ni wikiendi nzuri sana... sapoti ya ajabu kwa muda wote na ya kushangaza kuona mstari wa mwisho hapa, asante, kila mtu. Ina maana kubwa kama dereva wa Toyota kuendeleza ushindi huo hapa Safari. Ni muhimu sana kwa timu, wanafanya kazi kwa bidii kwa hili na wanastahili," alisema.

Elfin Evans alirekodi ushindi wa mfululizo kwa mara ya kwanza, akimaliza zaidi ya dakika moja mbele ya dereva wa Hyundai Muestonia Ott Tanak.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Tanak aliongoza mbio kabla ya kuvunja shimoni siku ya Ijumaa. Mshindi wa mwaka jana Thierry Neuville wa Hyundai alikuja katika nafasi ya tatu.

Dereva wa kumaliza Sami Pajari alikuwa wa nne, na Mjapani Takamoto Katsuta alimaliza wa tano. Wote wawili waliendesha Toyota.

Gregoire Munster wa Luxembourg alikuwa wa sita huku McErlean wa Ireland akimaliza wa Saba. Wote walikuwa na magari ya Ford.