
Sheikh Nasr ameeleza wazi kwamba siku kumi za mwisho ni muhimu zaid kwenye mfungo kwani hapo imani yako imeinuka na mwenyezi Mungu husamehe.
"Kikubwa katika siku hizi kumi za mwisho, ni kwamba mwenyezi Mungu ametoa ruksa kubwa na nafasi kubwa kwa yeyote mwenye kudai ama kutaka kumuomba na yeye atamjibu. Kwa hivyo ni fursa ambayo mtume anasema tuitumie kwa sababu mwenyezi Mungu katika siku hizi huteremka na kuuliza nani mwenye jambo lake," alieleza Yusuf.
"Nani Mwenye kutaka kuniomba ili mimi nimjibu. Waisilamu tunaomba, maanake sote tuna matatizo. Sote tuna vilio, sote tuna jambo la kumuomba mwenyezi Mungu," alieleza zaidi.
Akizungumza pia amewataka waisilamu kutumia muda wa usiku kusali zaidi ili kumuomba Mungu kama alivyofunza mtume.
"Katika mambo yetu mengi tuchukue nafasi hizi za usiku. Ambazo tunaambiwa kwamba akiweza mtu atumie usiku wote, na asipoweza atumie nusu yake, na asipoweza atumie hata robo yake. Ilimradi kwamba aitumie kumuomba Mungu jambo la kwanza, alafu pili kufanya mambo ya heri," alieleza zaidi."Mwenyezi Mungu ametuhimiza tufanye mema katika siku hizi, ili kwamba katika mema tupewe ziada ndo maana husali usiku."
Kwenye mafunzo na maelezo Sheikh Nasir afafanua kwamba wakati wa Usiku mwenyezi Mungu husamehe. Na msamaha wa dhambi unatokana mtu kuswali mbele za Mwenyezi Mungu.
"Mwisho kuna msamaha wa dhambi hiyo pia inatoka na mtu kuhuisha sala zae za usiku. Atakapokuwa ameswali atasamehewa. Kama alivyotufunza mtume kutufundisha katika hadithi yake kwamba Mwenye kusimama kisimamo cha kusali usiku katika ramadhani Mwenyezi Mungu atamsamehe.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!