Maafisa wa Polisi katika kituo cha polisi cha Naivasha eneo la Naivasha walimkamata Jmshukiwa kwa kwa madai ya kumiliki silaha hatari kinyume cha sheria.
Mshukiwa mwenye umri wa 30 alikamatwa na maafisa wa polisi kwa madai ya kumiliki Bunduki iliyokuwa na marisasi mawili taarifa hizo ziliwafikia maafisa wa usalama kufuatia Habari kutoka kwa raia.
Wakishughulikia Habari hizo kwa njia ya dharura maafisa wa polisi waliari fiwa kuwa raia mmoja Aliona mshukiwa mmoja akiwa amebeba marisasi katika baa moja ya Nyama CHOMA kinamba Naivasha.
Maafisa wa usalama waliweza kuchukua hatua za upesi ili kubaini na kumkamata mshukiwa kutoka mahali aliposemekana alikuwa bila kupoteza muda wala kulimatia.
Kulingana na ukaguzi wa kina uliofanywa na maafisa wa usalama wa kitengo cha DCI kuweza kutambua aina ya silaha ambazo mshukiwa alikuwa nazo ni kuwa ilibainika wazi kuwa mshukiwa alikuwa anamiliki bunduki ambayo ilikuwa na urefu wa milimita 7.62 na urefu wa marisasi yenye milimita 9.
Mshukiwa alipatikana na silaha hizo haramu bila kuwa na vyeti au vibali vya kumruhusu kumiliki silaha hizo na alikuwa anakusudia kufanya nini nazo? Maswali yaliulizwa yakimkosa majibu.
Mshukiwa baada ya kukamatwa alipelekwa katika kituo cha polisi cha Naivasha ambapo uchunguzi wa kina unaendelea kumhusu mshukiwa na baadaye ataweza kufikishwa mahakamani kujibu mashitaka baada ya uchunguzi kukamilika.
Maafisa wa DCI kwa ushiriano na wananchi mara nyingi wamekuwa macho na kuwahabarisha wananchi na kuwaarifu kuwa wawonapo jambo lolote ambalo si sawa na ambalo linatishia usalama wa taifa au wananchi wawe tayari kupiga ripoti kwa maafisa wa usalama kwa kutumia nambri ya simu 0800722203 bila malipo yoyote.
Kesi za wananchi kupatikanabna silaha hatari bila vibali maalumu zimekuwa zikikithiri na kuchochea wasiwasi na uwoga kwa wananchi huku wanaopatikana na silaha hizo wakikosa kufafanuani wapi wanakopta silaha hizi haramu ambazo serikali instahili iwe na uwezo kwa kufahamu ni akina nani wanaomiliki silaha hizo.
Juhudi za maafisa wa usalama kufanya bidii na juhudi za upesi kumkamata bwana Matu ni jambo ambalo linastahiki kupongezwa kwa dhati kuu ikizingatiwa kuwa kama mshukiwa huyo hangetambuliwa kutoka kwa wananchi angekuwa ni mwiba mkubwa sana kwa usalama wa wananchi kwa jumla.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!