
Ameeleza kwamba aliisha katika maisha magumu sana ya utotoni lakini kwa sasa anafanya kazi katika shirika linalowasaidia watoto walemavu.
Kubwa zaidi Eric ni muimbaji na muigizaji katika filamu. Kulingana na yeye maisha ya awali yalimpiga chenga zaidi kwani hayakuwa mepesi "Baba yangu alinikata kwa sababu ya ulemavu wangu,' alisema
WAkati huo ameelezea kwamba anapitia unyanyapaa kutoka kwatu wengine katika jamii hasa anaenda sehemu ambayo yeye ni mgeni au hajakutana na watu wa sehemu hiyo.
"Watu wanaoishi mbali na kwetu, wakiniona tu hushituka utafikiri kuna kitu cha ajabu ambacho kimetokea. Baadhi yao wananishangaa sana, wananitizama kama kitu cha ajabu," alisema
Baba alimchukia mama kwa sababu amemzaa mtoto kiwete mwenye ulemavu, wakaachana wakapeana talaka kwa sababu yangu. Nimekuwa katika maisha magumu sana niliwaita watoto wenzangu baba.
Mwanamziki huyo ambaye alizaliwa na ulemavu mkubwa alikiri kwamba changamoto kubwa katika maisha yake ilikuwa wakati wa kupata mke.
Kuna wale walionikubali na wengine walinikataa. Sio rahisi kwa sababu unapoishi na ulemavu na hata nyinyi mnafahamu kwamba ni tatizo. Tunaishi vizuri na mke wangu. Walosema walisema hata baada ya kuijfungua. Walisubiri waone kama nitapata mtoto mlemavu," aliweka wazi mwanamziki huyo.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!