
YOUTUBER na Rapa Diana Marua alinusurika kung’atwa na mbwa wake mguuni baada ya jaribio la kutaka kucheza na mbwa huyo kuenda fyongo.
Katika video ambayo alichapisha kwenye YouTube yake Ijumaa ya Machi 15, Marua ambaye alikuwa amevalia mavazi meusi alionekana akimkaribia mbwa huyo wanayemuita ‘Coco’.
Alikuwa akieleza mpango jinsi wanawe watakuwa wanamtoa mbwa wao kwenye nyumba yake mara kwa mara kwa ajili ya kumpigisha misele nje.
Hata hivyo, watoto hao walionekana kupinga wazo hilo tangu mwanzo, huku binti yake Heaven akilipinga kwa kauli kwamba mbwa wa familia ni mkali na anaweza dhuru watu.
Mama yao aliyeonekana kutoamini kauli za mwanaye kwamba mbwa wa familia ni mkali alitaka kuwaonyesha jinsi mbwa huyo ni rafiki kwa kila mtu – lakini jaribio lake nusra limsababishie kung’atwa.
kwa ujasiri alimuamuru mfanyakazi wao mmoja amwachie huru, lakini kabla hata mlango wa banda la mbwa haujafunguka, tayari watoto wake wote walikuwa wameshaingia ndani ya nyumba hiyo, na kumwacha Diana pekee ambaye ndiye aliyekuwa akimwonea huruma mbwa huyo, akiwa amesimama peke yake pale nje.
Wakati Coco alipoachiliwa, jambo lililomshtua sana Diana, badala ya kutoka nje kwa utulivu ili kufurahia uhuru wake, mbwa huyo alimfungia macho, akiwa na kasi kubwa, akibweka kwa hasira huku akimjia Diana kwa kasi.
Diana alijaribu kukwepa kasi ya mbwa wake ambaye alionekana kuwa na azma ya kufikia kisigino chake au paja lakini kwa Bahati nzuri, mfanyikazi wake ambaye alikuwa amemfungulia mbwa huyo alifika na kumzuia.
Marua alibaki katika hali ya mstuko na kutetemeka huku akiishiwa na maneno kinywani.
Baada ya kujikusanya Pamoja, Diana alikubaliana na wanawe kwamba mbwa huyo ni hatari kwa usalama wao pale nyumbani na kutoa maoni kwamba huenda wakawazia kumuuza ili kuleta mbwa mwingine mkarimu.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!