Thomas Tuchel ataja kikosi cha England

KOCHA wa timu ya taifa ya England, Thomas Tuchel ametaja kikosi chake katika kibarua chake cha kwanza tangu kuchukua mikoba ya ukufunzi wa Three Lions mapema mwaka huu.

Katika kikosi hicho, majina yaliyokuwa yamesahaulika yamerejeshwa tena kikosini huku wachezaji machipukizi pia wakipata wito kwa mara ya kwanza.

Mshambulizi wa Aston Villa Marcus Rashford ni miongoni mwa majina makubwa ambayo yamekuwa yakiachwa nje na mameneja wa awali.

Rashford aliichezea Uingereza mara ya mwisho katika mechi ya kirafiki dhidi ya Brazil mnamo Machi 2024 lakini amekuwa na kiwango kizuri tangu ajiunge na Villa kwa mkopo kutoka Manchester United mnamo Januari.

Mlinzi wa Newcastle Dan Burn na Myles Lewis-Skelly wa Arsenal wako kwenye mstari wa kucheza mechi zao za kwanza baada ya kuitwa kwa mara ya kwanza.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

England wanaanza kampeni yao ya kufuzu kwa Kombe la Dunia la 2026 kwa michuano miwili kwenye Uwanja wa Wembley dhidi ya Albania na Latvia siku ya Ijumaa, 21 na Jumatatu, 24 Machi mtawalia.

Rashford bado hajafunga bao katika klabu ya Villa lakini ameshapiga pasi nne za mabao huku akitaka kurejesha maisha yake ya soka.

Burn hajashiriki England katika kiwango chochote lakini amekuwa mchezaji wa kawaida na wa kudumu kwa Newcastle.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 32 anatoa uwezo wa kubadilika ikizingatiwa anaweza kucheza katikati ya safu ya ulinzi au beki wa kushoto.

Lewis-Skelly, 18, alicheza mechi yake ya kwanza ya ushindani akiwa na Arsenal mwezi Septemba lakini ameibuka kuwa mchezaji muhimu The Gunners.

Amekuwa akicheza nafasi ya beki wa kushoto lakini pia anaweza kucheza kiungo na amecheza mechi 25 msimu huu.

Kipa wa Burnley James Trafford na mlinzi wa Liverpool Jarell Quansah pia wanatumai kushinda mechi zao za kwanza za timu ya wakubwa.

Hiki hapa ndicho kikosi chote kwa ukamilifu:

Makipa: Dean Henderson (Crystal Palace), Jordan Pickford (Everton), Aaron Ramsdale (Southampton), James Trafford (Burnley)

Mabeki: Dan Burn (Newcastle United), Levi Colwill (Chelsea), Marc Guehi (Crystal Palace), Reece James (Chelsea), Ezri Konsa (Aston Villa), Myles Lewis-Skelly (Arsenal), Tino Livramento (Newcastle United), Jarell Quansah (Liverpool), Kyle Walker (AC Milan, mkopo kutoka Manchester City)

Viungo: Jude Bellingham (Real Madrid), Eberechi Eze (Crystal Palace), Jordan Henderson (Ajax), Curtis Jones (Liverpool), Cole Palmer (Chelsea), Declan Rice (Arsenal), Morgan Rogers (Aston Villa)

Washambuliaji: Jarrod Bowen (West Ham United), Phil Foden (Manchester City), Anthony Gordon (Newcastle United), Harry Kane (Bayern Munich), Marcus Rashford (Aston Villa, kwa mkopo kutoka Manchester United), Dominic Solanke (Tottenham Hotspur)