Washukiwa waliokamatwa na polisi

Polisi walianzisha msako mkali kufuatia msururu  wa wizi katika Barabara kuu  ya Thika mnamo Machi 11,2025 baada ya kundi la vijana kuvamia magari  na wasafiri baada ya mkutano wa Rais Ruto.

Katika taarifa iliyosomwa Alhamisi Machi 13,2025 kutoka kwa idara ya  upelelezi wa makosa ya Jinai DCI ilidhibitisha kuwa angalau  watu wanane walikamatwa kutokana na tukio hilo.

‘Kwa kujibu madai na tetesi kutokana na matukio  ya uvamizi na wizi yaliyotekelezwa na watu waliolenga  watu wasio na hatia  katika Barabara kuu ya Thika  mnamo Machi 11,2025 , Maafisa wa polisi wameanzisha  uchunguzi  wa kuwatambua wahalifu hao wote waliosababisha vitendo hivyo vyote vya uchama’  DCI  ilieleza.

DCI iliweza kumtambua mshukiwa mmoja kwa Jina Junior Odinga aliyekuwa amejihami kwa kisu  alipovamia raia mmoja na kumuibia simu aina ya Oppo A77S  iliyotoka shilingi elifu ishirini na nane 28,000.

‘’Oginga alikamatwa katika Barabara kuu ya Thika na kupelekwa  katika kituo cha polisi cha Pangani  taarifa ilieleza''.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Washukiwa wengine saba waliweza kukamatwa kutokana na msako mkali ulioendeshwa na maafisa wa polisi, waliokamatwa ni Jared Nyanza,Darlin Lande,Daniel Okombe,Mike Robert,Elvis Otieno,Reagan Omondi na Mathenge Gathiri hao walikamatwa kwa kuwaibia wapita njia katika eneo la Mathare mtaa wa 4( Mathare Area 4).

Washukiwa hao waliweza kupelekwa katika kituo cha polisi cha Muthaiga DCI ilieleza.Polisi waliweza kupata shati saba mpya ambazo zilikisiwa ziliibiwa kutoka kwa waathiriwa,DCI ilieleza kuwa washukiwa wote waliweza kukamatwa na kufikishwa katika vituo vya polisi ili kuandikisha taarifa.

Pikipiki nyingi zilionekana siku ya Jumanne Adhuhuri zilizowashutua wasafiri na watumizi wa Barabara kwa kusababisha hali ya wasiwasi na sintofahamu miongoni mwa wananchi.

Katika Video zilizoonekana katika  mitandao ya kijamii zilionyesha vijana  wengi  wakifunga sehemu za Barabara, kuwalazimisha wapitanjia kuwapa walivyokuwa wamebeba Pamoja na kuwaibia waliokuwa ndani ya magari ya binafsi.

Walekwa wa matukio hayo walipata wakati  mgumu kuweza kujinasua kutoka kwa wahuni hao huku tahadhari ya kutotumia Barabara hiyo ikisambazwa mitandaoni kuwaonya wananchi kutotumia Barabara hiyo.

’Kwa sasa wasafiri muepuke kutumia Barabara kuu  ya Thika katika mpitio wa Barabara ya wasafiri wa miguu ya  KCA kuna kundi la Vijana amabalo linawaibia watu na hata kuingia kwenye magari ya umma Huduma ya polisi kwa umma tunataka  usaidizi wenu maelezo kutoka kwa Sikika Usalama Kwa Barabara(Sikika Road Safety) yalichapishwa katika ukurasa wao wa Facebook mnamo Machi 11,2025’’.