Marekani yasema iko huru kuchunguza  ushirikiano wa raslimali muhimu ya madini na serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo(DRC).

Huku Kongo ikitaka usaidizi wa Marekani  katika vita vyake vinavyoendelea dhidi ya waasi wanaodhibiti asilimia 10% ya eneo la Jamhuri ya Kidemokrrasia ya Kongo kulingana na mujibu wa ripoti kutoka Kinshasha.

Hatua hio inafuatia Kinshasa kutangaza Mipango ya kuimarisha jeshi katika suala la fedha na silaha na kuiwezesha kutekeleza hilo.

DRC ambayo ina utajiri  mkubwa wa madini ya Kobalti,Lithiamu na Uraniam miongoni mwa madini mengine imekuwa ikipambana na waasi wa M23 wanaungwa mkono na na nchi ya Rwanda ambayo imeteka maeneo mengi mwaka huu.

Katika ushirikiano huu serikali ya Kinshasa inapania kuzipa kampuni za Marekani haki ya kuchimba na kusindika madini ya thamani na kulipia msaada huo.  Serikali ya Kinshasha ilihitaji msaada  wa kijeshi,mafunzo Pamoja na vifaa vya kijeshi.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Mwishoni mwa mwezi uliopita serikali ya Kinshasa iliiomba Marekani kuwekeza katika nchi yenye hifadhi ya madini ya thamani ya  dola trilioni 24 ambazo hazijatumiwa .

Madini ni muhimu kijeshi,Kiteknologia na nishati  kulingana na barua ya serikali ya Kinshasa kwa serikali ya Marekani.

‘’ Kuna nia ya sisi kubadilisha washirika wetu’’ msemaji wa serikali ya DRC Patrick Muyaya alisema juma lililopita.

‘’Ikiwa leo wawekezaji wa Marekani wana nia ya kuja DRC  ni wazi watapata nafasi DRC ina akiba ambayo inapatikana na itakuwa vizuri kama mitaji ya Marejkani inaweza kuekeza hapa ‘’alisema.

Barua ya DRC inaomba kwamba Rais Trump wa Marekani binafsi awepo   kwenye mijadala kuhusu ushirikiano huu na kuamba mkutano kati ya Rais Trump na rais Tshisekedi  utakuwa muhimu katika kufanikisha ushirikiano huo.

Akielezea kuhusu ushirikiano wa Marekani na DRC Tina Salama msemaji wa Rais Tshisekedi aliandika kwenye ukurasa wa X kwamba Tshisekedi alialika Marekani  yenye kampuni zinazonunua  vifaa vya msingi kutoka Rwanda  vinavyoporwa nchini DRC  na kuingizwa nchini Rwanda ambapo kwa sasa wanaiomba Marekani inunue kutoka kwa mmiliki halisi wa madini.

Kwa upande mwingine Rwanda ilisema kuwa madini ya DRC si sababu ya mzozo wake na DRC na kwamba   wanaochimba na kufaidika   nayo ni Kampuni kutoka magharibi. Rwanda pia ilikanusha  kusaidia kundi la waasi wa m23.