Marekani yasema iko huru kuchunguza ushirikiano wa raslimali muhimu ya madini na serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo(DRC).
Huku Kongo ikitaka usaidizi wa Marekani katika vita vyake vinavyoendelea dhidi ya waasi wanaodhibiti asilimia 10% ya eneo la Jamhuri ya Kidemokrrasia ya Kongo kulingana na mujibu wa ripoti kutoka Kinshasha.
Hatua hio inafuatia Kinshasa kutangaza Mipango ya kuimarisha jeshi katika suala la fedha na silaha na kuiwezesha kutekeleza hilo.
DRC ambayo ina utajiri mkubwa wa madini ya Kobalti,Lithiamu na Uraniam miongoni mwa madini mengine imekuwa ikipambana na waasi wa M23 wanaungwa mkono na na nchi ya Rwanda ambayo imeteka maeneo mengi mwaka huu.
Katika ushirikiano huu serikali ya Kinshasa inapania kuzipa kampuni za Marekani haki ya kuchimba na kusindika madini ya thamani na kulipia msaada huo. Serikali ya Kinshasha ilihitaji msaada wa kijeshi,mafunzo Pamoja na vifaa vya kijeshi.
Mwishoni mwa mwezi uliopita serikali ya Kinshasa iliiomba Marekani kuwekeza katika nchi yenye hifadhi ya madini ya thamani ya dola trilioni 24 ambazo hazijatumiwa .
Madini ni muhimu kijeshi,Kiteknologia na nishati kulingana na barua ya serikali ya Kinshasa kwa serikali ya Marekani.
‘’ Kuna nia ya sisi kubadilisha washirika wetu’’ msemaji wa serikali ya DRC Patrick Muyaya alisema juma lililopita.
‘’Ikiwa leo wawekezaji wa Marekani wana nia ya kuja DRC ni wazi watapata nafasi DRC ina akiba ambayo inapatikana na itakuwa vizuri kama mitaji ya Marejkani inaweza kuekeza hapa ‘’alisema.
Barua ya DRC inaomba kwamba Rais Trump wa Marekani binafsi awepo kwenye mijadala kuhusu ushirikiano huu na kuamba mkutano kati ya Rais Trump na rais Tshisekedi utakuwa muhimu katika kufanikisha ushirikiano huo.
Akielezea kuhusu ushirikiano wa Marekani na DRC Tina Salama msemaji wa Rais Tshisekedi aliandika kwenye ukurasa wa X kwamba Tshisekedi alialika Marekani yenye kampuni zinazonunua vifaa vya msingi kutoka Rwanda vinavyoporwa nchini DRC na kuingizwa nchini Rwanda ambapo kwa sasa wanaiomba Marekani inunue kutoka kwa mmiliki halisi wa madini.
Kwa upande mwingine Rwanda ilisema kuwa madini ya DRC si sababu ya mzozo wake na DRC na kwamba wanaochimba na kufaidika nayo ni Kampuni kutoka magharibi. Rwanda pia ilikanusha kusaidia kundi la waasi wa m23.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!