Haijabainika kwa muda gani mtuhumiwa aliendesha kituo hicho cha polisi.
Polisi walisema waligundua kuwa kituo hicho kilikuwa kinafanya kazi bila idhini ya mamlaka mnamo Machi 8 saa tano asubuhi.
Mtuhumiwa ni mkazi wa kijiji cha Asis, eneo la Ndugulu, tarafa ya Kesses, kaunti ya Uasin Gishu.
Alifanya uamuzi wa kuanzisha kituo cha doria ya polisi ndani ya mtaa wa Cherus, katika moja ya majengo ya mwenye nyumba, kwa kukipaka rangi za jeshi la polisi.
Advertisement
Advertisement
Alifanya hivyo bila ufahamu wa maafisa wakuu wa polisi, hali iliyosababisha uchunguzi wa kina kufanyika.