Mtu mnene kupindukia

SHIRIKA la kutoa taarifa kuhusu unene wa kupindukia duniani limeonya kwamba huenda idadiv ya watu wazima wanaoishi na unene wa kupindukia ikaongezeka kutoka milioni 524 hadi bilioni 1.13 kufikia mwaka wa 2030.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo ambayo imechapishwa kwenye Tovuti ya World Obesity Atlas mnamo Machi 5, mataifa mengi ikiwemo Kenya hayako tayari kuweka mikakati ya kuzuia ongezeko la unene kupitia kiasi.

“Nchi nyingi duniani hazina mipango na sera za kutosha za kukabiliana na ongezeko la viwango vya unene wa kupindukia,”

“Atlas yetu ya 2025 World Obesity Atlas, iliyochapishwa kwenye Siku ya Uzito Duniani, (4 Machi), miradi ambayo jumla ya watu wazima wanaoishi na unene itaongezeka kwa zaidi ya 115% kati ya 2010 na 2030, kutoka milioni 524 hadi bilioni 1.13,” ripoti hiyo ilionya.

Shirika hilo lilitoa wito kwa serikali za mataifa yote kuchukulia suala la ongezeko wa unene wa mwili kupindukia kama jukumu la jamii nzima.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Shirika hilo lilionya kwamba iwapo watu wazima wataendelea kuendekeza unene wa kupindukia, basi katika kipindi cha miaka 5 ijayo idadi ya wenye unene wa kupindukia itakuwa mara mbili zaidi ya ilivyo sasa.

“Tunatoa wito kwa serikali kushughulikia suala la unene wa kupindukia kama suala la 'jamii nzima', kwa kuanzisha sera ikiwa ni pamoja na kuweka lebo na ushuru wa chakula, kwa kuunda mazingira yaliyojengwa ambayo yanahimiza mazoezi ya mwili, na kwa kuimarisha mifumo ya afya ili kutoa huduma ya afya ya unene uliozingatia watu.”

“Viwango vya unene wa kupindukia vya Daraja la II na zaidi (BMI zaidi ya kilo 35/m2) - kiwango cha kawaida kinachotumika wakati matibabu yanapendekezwa - imewekwa kuwa zaidi ya maradufu kote ulimwenguni kufikia 2030, huku watu wazima 385m wakifikia fahirisi ya uzito wa mwili zaidi ya 35kg m2, kutoka 157m mnamo 2010,” walieleza.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo, Ongezeko la ugonjwa wa kunona kupita kiasi na magonjwa yanayotokana na ugonjwa huo yanatokea kwa kasi zaidi katika nchi zenye kipato cha chini na cha kati, ambazo huwa haziko tayari kukabiliana na ongezeko la viwango vya unene wa kupindukia, hasa linapokuja suala la mifumo ya afya.