
MWALIMU wa zamani wa PE aliyeacha kazi yake baada ya miaka na kukumbatia kazi ya kuosha na kuhifadhi maiti amesimulia jinsi haikumkalia viguku kuchukua maamuzi hayo ya kubadilisha taaluma.
John Redhead, kutoka Ripley huko Derbyshire nchini Uingereza, kwa sasa anafanya mafunzo na hospitali moja ili kuwa msafishaji wa maiti aliyehitimu huku mitihani yake ya nyanjani ya miaka miwili ikitarajiwa kuanza mwezi Juni.
Mzee huyo mwenye umri wa miaka 46 alisema ujuzi wa kujali aliojifunza kutoka miaka 22 katika elimu ulihamia vyema kwenye tasnia ya maziko.
Wakati akiacha kufundisha "ilikuwa mojawapo ya maamuzi magumu zaidi ambayo nimewahi kufanya", alisema alikuwa akifurahia maisha yake mapya.
"Siku zote nilifurahia sana kipengele cha uchungaji cha jukumu langu kama mwalimu, lakini ilianza kuhisi kama kazi ilikuwa ya kupata matokeo, na thamani ya kila mwanafunzi kulingana na mafanikio yao ya kitaaluma," aliiambia BBC Radio Derby.
"Niliacha kufundisha bila kupangiwa kazi nyingine, kwa hivyo nilifikiria ni ujuzi gani ninao kutoka kufundisha hadi jukumu jipya.”
Bw Redhead alisema alitumia ramani ya matrix ya ujuzi, ambayo hutumia ujuzi na viwango vya ujuzi wa mtu kutoka kazi za awali na kulinganisha ujuzi huo na kazi mpya.
Alisema matrix ya ujuzi ilimpa "mawazo mengi" lakini machapisho ya mitandao ya kijamii kuhusu kufanya kazi katika makafani yaliendelea kuonekana kwenye simu yake, ambayo ilimsaidia kuchagua kazi yake mpya.
"Baada ya kupata matokeo kutoka kwa matrix ya ujuzi wangu, nilienda kwa fayre ya kazi na ikatoka hapo," alisema.
Kuweka maiti ni mchakato wa kuhifadhi mwili baada ya kifo na kabla ya mazishi yao.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!