
Selebwa alisisitiza kuwa ndugu hao wawili waliweka kiwango cha juu katika soka la Kenya na wanapaswa kuwa chachu kwa wachezaji chipukizi na juhudi za kufufua uwezo wa soka wa Busia.
Busia ni kitovu cha talanta. Mchezaji wa kwanza wa Kenya na Afrika Mashariki kushiriki katika UEFA Champions League alikuwa McDonald Mariga, na Mkenya wa kwanza kucheza Ligi Kuu ya Uingereza alikuwa Victor Wanyama. Hii peke yake inathibitisha kuwa Busia ina uwezo wa kuunda soka la Kenya," alisema Selebwa.
Pia ametaka juhudi mpya za kurejesha sifa ya Busia kama wachezaji wenye nguvu ya mpira wa miguu kukumbatiwa. Amezungumza huku akikumbuka enzi za Wilberforce Mulamba, ambaye alikuwa miongoni mwa vipaji bora vya AFC Leopards pamoja na JJ Masiga, Noah Wanyama na Francis Barasa.
Ukiangalia nyuma, utaona wachezaji wengi kutoka Busia ambao waliwakilisha nchi vizuri sana hasa katikampira wa kandanda.
"Tunaweza kujivunia kusema Busia ni nyumbani kwa vipaji vikubwa, lakini lazima tuhakikishe timu zetu zinashindana katika Ligi Kuu ya Kenya. Inasikitisha kwamba hakuna timu kutoka Busia inayoshiriki KPL kwa sasa, ikimaanisha hakuna mechi za Ligi Kuu zinazoandaliwa katika eneo hilo," Selebwa alibainisha.
Kwa sasa kocha mkuu wa HOHA FC, Selebwa amejikita zaidi kuisaidia timu yake kupata nafasi ya kupanda daraja kutoka FKF Division One hadi Ligi Kuu ya Taifa (NSL), huku lengo kuu likiwa ni kufikia Ligi Kuu ya KPL..
Mariga kwa sasa ndiye naibu mwenyekiti wa FKF nchini huku Wanyama pia akiwa amesitaafu .
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!