February 5, 2025
2 min read
Afisa aliyehusika na
kucheza wimbo usio sahihi wa taifa la Kenya kabla ya mechi dhidi ya Uganda
katika michuano ya kufuzu kwa FIBA Women's AfroBasket 2025 amepigwa kalamu.
Tukio hilo lilitokea
Februari 3, 2025, jijini Cairo, Misri, ambapo wimbo huo ulidumu kwa sekunde 19
kabla ya kusitishwa, hali iliyowaacha wachezaji wa Kenya wakiwa na huzuni.
Wachezaji wa Kenya
walionekana kupinga wimbo wa taifa usio sahihi na kutaka usimamishwe ulipokuwa
ukicheza. Wimbo wa taifa usio sahihi ulisitishwa baada ya takriban sekunde 20
na ule sahihi ukachezwa kufuatia pingamizi kali la wachezaji.
Siku ya Jumanne, Chama
cha Kitaifa cha Mpira wa Kikapu cha Kenya (NBA Kenya) kilitoa taarifa kikieleza
kuwa ripoti rasmi kuhusu tukio hilo imewasilishwa kwa Shirikisho la Mpira wa
Kikapu Duniani (FIBA) kwa hatua zaidi.
Enjoying this article?
Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans
“Mtu aliyehusika
kucheza wimbo wa taifa usio sahihi katika mchezo wa Kenya dhidi ya Uganda
katika Mashindano ya kufuzu kwa Afrobasket ya FIBA kwa Wanawake, amefukuzwa
kazi na ripoti kuandikiwa FIBA," NBA Kenya ilisema katika taarifa yake.
Timu ya taifa ya Kenya
(Lionesses) ambayo inanuia kufuzu kwa mashindano ya mwaka huu iliishia
kupoteza mchuano huo dhidi ya Uganda, 78-56.
Timu hiyo iliendelea na
mwanzo wake hafifu siku ya Jumanne, Februari 5, 2025, waliposhindwa na Sudan
Kusini 86-69 katika mechi yao ya awamu ya pili ya ligi iliyochezwa Cairo,
Misri.
Hiki kilikuwa kipigo
cha pili kwa Lioness, baada ya kupoteza mchuano wao wa kwanza wa awamu ya
makundi dhidi ya Uganda.
Mashindano ya Awali ya
Mchujo ya FIBA ya Wanawake wa AfroBasket 2025 Zone 5, yaliyoanza Februari 3,
2025, yataendelea hadi Februari 8, 2025, kwenye Ukumbi wa Hassan Mostafa Arena
huko Giza, Misri.
Mataifa sita—Misri,
Kenya, Burundi, Tanzania, Sudan Kusini, na Uganda—yanashindana kwa nafasi
inayotamaniwa katika FIBA Women’s AfroBasket 2025, iliyoratibiwa kufanyika
nchini Côte d’Ivoire.
Lionesses wamepangwa
pamoja na nchi mwenyeji Misri, Uganda, Burundi, na Sudan Kusini katika
mazingira ya kushinda au-kwenda nyumbani huku wakiwania tiketi ya mchuano wa
kuwania ubingwa wa bara hilo nchini Côte d'Ivoire.
Mashindano haya
yanaendelea huku timu zikijitahidi kupata nafasi ya kufuzu kwa michuano ya FIBA
Women's AfroBasket 2025.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!