RAPA King Kaka amebaki kinywa wazi baada ya kuyakuta yasiyoweza kusemeka kwenye mtandao wa TikTok.
Msanii huyo ambaye waliachana na mkewe mwishoni mwa mwaka jana alishangaa baada ya shabiki wa kike kujitokeza kimasomaso akimtaka kumpa mimba.
Kilichomshangaza zaidi ni kwamba huyo shabiki alimpa masharti ya kumpa mimba na kisha baadae aikatae endapo atamtafute kumjulisha kuhusu mimba yake.
“King Kaka kuja unipe mimba halafu uiruke,” Shabiki huyo kwa jina Ezna alimrai Msanii huyo.
Baada ya kupatana na maoni hayo miongoni mwa watu zaidi ya elfu 12 kwenye kipindi cha moja kwa moja katika ukurasa wake wa TikTok, King Kaka alibaki akishangaa na kusema ‘wuueh’.
Alipochapisha maoni hayo kwenye ukurasa wake wa Instagram, watu walitoa maoni baadhi wakimshauri kumfanyia haki Ezna na wengine wakisema kwamba hu oni mtego.
Haya hapa ndio maoni ya baadhi ya watu kwenye ukurasa wake wa Instagram;
@khoerose8: “Lakini King Kaka huwa ni mali safi tuseme ukweli tu.”
@_j.o.j.i_: “Anadhani utaruka juu wewe ni sungura.”
@_.jokul_: “Hivyo ndio wao husema halafu baadae unakuwa baba asiyetoa msaada katika malezi.”
@mona_binti_ali: “Wacha watakuanika huku mitandaoni kama baba aliyekufa.”
@sue_oduya: “Halafu yeye ndio ataenda kupea yule Obare chai eti wewe ni deadbeat.”
Maoni yak oni yepi kuhusu suala la shabiki kumuomba msanii wake pendwa fadhila ya kupewa mimba?
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!