Karoline Leavitt Katibu wa Habari ya White House ya Marekani ndiye mdogo zaidi kihisitoria kushikilia wadhifa huo.
Anatarajiwa kutoa taarifa yake ya kwanza kwa vyombo vya habari siku ya Jumatano
Kijana huyo mwenye umri wa miaka 27, ambaye alikuwa msemaji wa kampeni za Donald Trump, anatarajiwa kuanza kazi yake ya kwanza kutua jukwaani katika wiki ya pili ya rais huyo baada ya kurudi madarakani.
Mkutano wa kwanza wa utawala mpya ni wakati mkubwa, kwani katibu wa habari za Ikulu atakutana ana kwa ana na vyombo vya habari.
Waziri wa kwanza wa habari wa Trump wakati wa muhula wake wa kwanza, Sean Spicer, alisababisha utata katika mkutano wake wa kwanza, kwa kuchochea makadirio ya ukubwa wa umati wakati wa kuapishwa na kusema kwamba White House wakati mwingine inaweza "kukubaliana na ukweli"
Akitangaza Leavitt kama chaguo lake mwezi Novemba, Trump alisema kuwa ana imani mgombea huyo wa wakati mmoja wa Congress - ambaye pia alihudumu katika ofisi ya habari ya White House wakati wa utawala wa kwanza wa Trump - "atafika jukwaani na kusaidia kufikisha ujumbe wetu kwa watu wa Marekani tunapoifanya Marekani kuwa kubwa tena".
"Karoline ni mwerevu, mgumu, na amethibitika kuwa mtu mwenye ufanisi mkubwa," Trump alisema.
Mzaliwa wa New Hampshire, Leavitt alisoma mawasiliano na sayansi ya siasa katika Chuo cha Saint Anselm, chuo cha Kikatoliki katika jimbo lake la nyumbani.
Akiwa bado shuleni, alisomea katika kituo cha habari cha Fox News na kufanya katika ofisi ya habari ya Trump White House.
Aliiambia Politico mnamo 2020 kwamba alipata "mtazamo wake wa kwanza katika ulimwengu wa vyombo vya habari" kupitia uzoefu huo, ulisababisha uamuzi wake wa kufuata kazi katika mahusiano ya vyombo vya habari, alisema.
Leavitt alianza kufanya kazi katika ikulu ya kwanza ya Trump muda mfupi baada ya kuhitimu mwaka 2019.
Kwanza kama mwandishi wa hotuba ya rais na baadaye kama katibu msaidizi wa vyombo vya habari,kwa mujibu wa tovuti ya kampeni yake ya kuwania urais mwaka 2022.
"Nilisaidia kuandaa Katibu wa Habari Kayleigh McEnaney kwa ajili ya mikutano wa shinikizo kubwa na kushindana dhidi ya vyombo vya habari vya kawaida," tovuti yake ilisema.
Baada ya kuondoka White House, Leavitt aliwahi kuwa mkurugenzi wa mawasiliano wa Elise Stefanik, mbunge mwandamizi wa Republican ambaye Rais mteule Trump amemteua kuwa balozi wa Umoja wa Mataifa.
Leavitt aliacha jukumu hilo na kugombea ubunge, akishinda uteuzi wa Republican kwa wilaya ya bunge la New Hampshire mwaka 2022, na akapoteza katika uchaguzi mkuu kwa Mdemokrat Chris Pappas.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!