
Waziri wa Masuala ya Vijana, Uchumi wa Ubunifu na Michezo Salim Mvurya amewahakikishia Wakenya kwamba Uwanja wa Talanta Sports City unaoendelea kujengwa utakuwa tayari kufikia Desemba mwaka huu.
Siku ya Alhamisi, gavana huyo wa zamani wa Taita Taveta alifanya ziara ya kwanza katika kituo hicho tangu alipochukua wizara ya michezo mapema mwaka huu na alionyesha kuridhishwa kwake na kazi za mkandarasi wa China ,China Road and Bridge Corporation.
Waziri pia alielezea kuridhishwa kwake na kazi ya ukarabati na uboreshaji inayoendelea katika viwanja vya Nyayo na Kasarani.
"Kutokana na maelezo mafupi na nilichoona, uwanja utakuwa tayari Desemba. Nimefurahishwa na maendeleo na pia na viwanja vingine (Nyayo na Kasarani). Kuna kazi nyingi inayoendelea katika idara zote kama vile viingilio na stendi ya VIP, kwa hivyo inaendelea vizuri na itakuwa tayari kwa wakati," Mvurya alisema baada ya ukaguzi huo.
Kwa sasa, Uwanja wa Talanta uko kwenye daraja la tatu kwa ujenzi.
“Mashabiki wengi wa soka nchini wanafuatilia kwa makini maendeleo ya kituo hiki kwa sababu sisi (Kenya) pamoja na Tanzania na Uganda tutaandaa michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika 2027, nikiwa waziri wao, ninawahakikishia tutakuwa tayari na watafurahia mchezo wa soka,” aliongeza waziri huyo.
Uwanja wa Talanta Sports City ambao unajengwa kwenye shamba la hekta 45.64 kando ya Barabara ya Ngong ya Nairobi, utakuwa na uwanja wa mazoezi wa nje, uwanja wa kawaida wa riadha na uwanja mmoja wa mazoezi wa raga.
Baada ya kukamilika, uwanja huo mzuri wa michezo unatarajiwa kuwa na uwezo wa kubeba takriban watu 60,000, na kuufanya kuwa karibu ukubwa sawa na uwanja wa Kasarani.
Ni jambo la kusisimua kufahamu kuwa uwanja huo unaotarajiwa kutumika kwa AFCON 2027 utakuwa mkubwa kuliko baadhi ya viwanja maarufu barani Ulaya. Angalia hapa chini baadhi ya viwanja vya Ulaya vyenye uwezo wa kubeba watu wasiozidi 60,000.
Viwanja maarufu Ulaya ambavyo ni vidogo kuliko Uwanja wa Talanta
*Uwanja wa Talanta unakadirwa kukamilika Desemba 2025 na utabeba watu 60,000*
>Stadio Diego Armando Maradona (Napoli)
54,720
> Uwanja wa Etihad (Man City) - 52, 900
> St. James Park (Newcastle) - 52, 250
>Parc des Princes (PSG) -48,527
>Villa Park (Aston Villa) - 42,910
>Uwanja wa Juventus (Juventus) - 41,500
>Stamford Bridge (Chelsea) - 40,173
>Goodison Park (Everton) - 39,410
> King Power (Leicester) - 32,260
>Stade Louis II (Monaco) - 18, 520
Chanzo: Stadium Guide
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!