TIKTOKER Rachael Otuoma amefunguka hatua ambazo anataka kuzichukua ili kujiepusha na mawazo mengi kuhusu kufiwa na mumewe, mwanasoka Ezekiel Otuoma.


Kupitia mitandao wa TikTok, mrembo huyo ambaye alimzika mumewe takribani wiki mbili zilizopita alitangaza kwamba haijakuwa rahisi kuishi bila kipenzi cha moyo wake.


Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Rachael alisema kwamba ameona akiendelea kukaa tu bure atajikuta amezama kwenye lindi la mawazo na unyongovu, akisema kwamba sasa inambidi aanze kutafuta kazi za taaluma yake ya kurembesha nyumba ndani.


Mrembo huyo pia alitangaza kwamba anachukua likizo kutoka kwenye mitandao huo na kwenda kuzikata nywele zake na wakati atakaporudi, kichwa chake kitakuwa na mfanano wa jinsi mumewe alikuwa anapenda kunyoa.


“Naenda kunyoa, nikirudi nitakaa Otuoma kabisa. Nataka kunyoa ule mtindo kama wa Otuoma. Mnaona ile staili Otuoma alikuwa ananyoa halafu anaweka rugged hapa juu, hiyo. Unajua sasa hivi mtu unafaa kufanya kile kitu ambacho kitakufanya ukuwe na furaha,” Rachael alisema.


Kando na kunyoa, mrembo huyo pia alisema yuko katika harakati za kutafuta makazi mapya na kuhama katika ile nyumba ambamo walikuwa wanaiashi na marehemu Ezekiel Otuoma.


Rachael alisema licha ya kuhama, hatouza au kupeana kiti ambacho Otuoma alikuwa anapenda kukalia kwa nyumba, akiweka wazi kwamba mwishoni mwa mwezi huu atakuwa amefanikisha kuhama.


“Mawazo yataniua, kusema ukweli nikikaa kwa nyumba tu hivi kila wakati nafikiria sana. Nikipiga kona hivi naona picha ya Otuoma ikinitabasamia, huku kwingine naona Otuoma na mimi vile alikuwa anatabasamu kwa kile kiti chake pale. Hiki kiti sitapeana, nataka tu kutafuta kazi niwe busy.”


“Jumatano niko na kazi moja na lazima nitaenda kwa sababu kukaa tu hivi mawazo yataniua. Nitakufa na stress. Kuhama nitahama hivi karibuni, mwishoni mwa mwezi huu. Nitatoka hapa,” Rachael alisisitiza.


Mwanasoka huyo alifariki mwishoni mwa mwaka jana, siku chache tu kuelekea sikukuu ya Krismasi na kuzikwa wiki ya kwanza ya Januari mwaka huu.


Kabla ya kifo chake, Otuoma alipigana vita dhidi ya ugonjwa wa Motor Neurone ambao unaathiri neva za mwili kwa kipindi cha miaka4 tangia mwaka 2020.