CHIEF GODLOVE Mwakibete, kijana mdogo mwenye utajiri wa kushangaza kutoka nchini Tanzania ameibuka na mapya akiwajibu mbona mara nyingi huwa hasafiri nje ya nchi.
Kijana huyo ambaye ameibukia kuwa gumzo kubwa mitandaoni miezi ya hivi karibuni kutokana na utajiri wake, alisema kwamba amekuwa akipata maswali mengi kutoka kwa watu wanaohoji mbona huwa hasafiri kwenda kula bata katika mataifa na miji ya kitajiri kama vile Dubai na Marekani kama matajiri wenzake.
Akijibu swali hilo kwa utani, Godlove alisema kwamba hawezi kusafiri kuenda Dubai na Marekani kujivinjari kama matajiri wenzake, kwa vile hakuna mtu atakayeachia nyoka wake kumlisha.
“Mnaouliza mbona siendi Dubai na Marekani, nyoka mtalisha nyinyi? Kwendeni zenu, siendi Marekani wala Dubai, majini yangu na mizimu atalisha nani?” Godlove alijibu kwa utani usio wa kawaida.
Hata hivyo, kijana huyo alifuta chapisho hilo baadae kutoka kwenye kurasa zake za Instagram na X alikokuwa amezichapisha siku ya Alhamisi.
Jibu hilo, japo lilikuwa la kitani, lakini lilionekana kuzua maswali mengi kuliko majibu miongoni mwa watu anaowatia moyo katika safari ya kutafuta utajiri.
Hii si mara ya kwanza kwa mkwasi huyo mchanga kutoa kauli za kutatanisha kuhusu Imani yake katika utajiri na Uuungu.
Siku chache zilizopita, Godlove alionekana kutilia shaka uwepo wa mbinguni, akisema kwamba viongozi wa kidini wanaotangaza Habari za mbinguni hata wao wenyewe hawaijui.
“Ukitaka Habari za kwenda mbinguni hata anaekusisimulia Habari za huko ajawahi kwenda fuatilia wachungaji na mashekhe ukitaka kujitambua wewe ninani umezaliwa kufanya nini ili ufanikiwe Kua na uwezo wa kujitibu na kujiombea nisikilize kisha fuata nnachokuelekeza mimi,” Godlove aliandika kwenye X, Januari 3.
Mwaka 2025 ulipoanza, Chief Godlove alisema kwamba ombi lake kuu mwaka huu ni Mungu kumwepushia wanawake wasiopenda hela kwani watamfanya kuwa mzembe wa kuzitafuta.
“Mwaka 2025 mungu niepushie wanawake wasiopenda pesa watanifanya niwe maskini,” aliomba.
Katika
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!