KLABU YA EVERTON imekuwa ya hivi punde kwenye ligi kuu ya premia nchini Uingereza kufuta kocha wa kikosi cha kwanza.
Klabu hiyo ya Merseyside ilitoa taarifa ya kumfukuza kazi kocha Sean Dyche usiku wa Alhamisi kufuatia msururu wa matokeo duni.
Sean Dyche anaondoka baada ya kushinda mechi moja pekee katika mechi 11 zilizopita, na kuwaacha pointi moja juu ya eneo la kushuka daraja la Ligi Kuu.
Leighton Baines na Seamus Coleman wanatazamiwa kutwaa usukani wa mechi ya raundi ya tatu ya Kombe la FA dhidi ya Peterborough Alhamisi jioni.
The Toffees wako katika nafasi ya 16 kwenye Premier League na hawakupiga shuti lililolenga lango wakati wa kupoteza kwa 1-0 Jumamosi dhidi ya Bournemouth - kipigo chao cha nane kwenye ligi msimu huu na wameshindwa kufunga katika mechi nane kati ya 10 zilizopita.
Kufutwa kwa Dyche kunajiri siku moja tu baada ya wenzao West Ham kumfuta kocha Julen Lopetangui.
Nafasi yake ilichukuliwa na kocha wa zamani wa Chelsea na Brighton, Graham Potter ambaye atakuwa West Ham kwa mkataba wa miaka miwili na nusu.
Desemba 15, Southampton walitangaza kumfuta kocha wao Russell Martin kufuatia timu hiyo kuanza vibaya msimu wa Ligi ya Premia, ambayo ilifikia kilele kwa kushindwa kwa mabao 5-0 dhidi ya Tottenham Hotspur siku ya Jumapili.
Mkufunzi huyo mwenye umri wa miaka 38 anaondoka kwenye mkia wa klabu na tayari pointi tisa kutoka kwa usalama akiwa amechukua pointi tano kutoka kwa michezo 16.
Desemba 16, Wolves ilimfuta kazi kocha mkuu Gary O'Neil baada ya kushindwa nyumbani na Ipswich - na wako kwenye mazungumzo na meneja wa Ureno Vitor Pereira kuchukua nafasi yake.
O'Neil alitimuliwa baada ya kupoteza kwa mabao 2-1 dhidi ya Molineux, ambayo ilifuatiwa na pambano lililomfanya Rayan Ait-Nouri kutolewa nje ya uwanja.
Mwezi Novemba, Leicester walimtimua meneja Steve Cooper baada ya kuifundisha kwa miezi mitano pekee kufuatia kipigo cha mabao 2-1 kutoka kwa Chelsea.
Bosi huyo wa zamani wa Nottingham Forest alijiunga na Foxes kwa mkataba wa miaka mitatu mwezi Juni lakini amefukuzwa kazi baada ya kushinda mechi tano bila kushinda katika mashindano yote.
Manchester United walikuwa wa kwanza kumfuta kazi kocha wao, ERIK Ten Hag mwezi Oktoba kufuatia msururu wa matokeo duni.
Mchezo wa mwisho wa Ten Hag ulikuwa wa kushindwa mabao 2-1 dhidi ya West Ham na kuiacha klabu hiyo ikiwa nafasi ya 14 kwenye Ligi Kuu ya England ikiwa na ushindi mara tatu pekee katika mechi tisa za mwanzo.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!