MCHEKESHAJI Kendrick Mulamwah kwa mara ya kwanza amevunja kimya kuhusu madai yanayoendelea mtandaoni kuusu gari lake kupigwa mnada lakini pia kuwa na deni kubwa la benki.


Madai hayo yamekuwa yakienezwa katika mitandao ya kijamii tangu mwaka uanze na chanzo chake hakijulikani, huku kila mtu akionekana kuwa na maoni yake kuhusu suala hilo.


Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Hata hivyo, kupitia ukurasa wake wa Facebook, Mulamwah alizungumzia suala hilo kwa mara ya kwanza baada ya kugundua kwamba lilikuwa suala la mjadala pevu katika ukurasa mmoja kwenye TikTok.


Mtu mmoja kwenye TikTok hata alidai kwamba Mulamwah anadaiwa na benki zaidi ya shilingi milioni 35 ambazo mtu huyo alidai kuwa alizitumia kujenga nyumba na kununua gari.


Hata hivyo, Mulamwah aliyeonekana kushangazwa na suala hilo alipigwa na butwaa kuona mtu huyo akiorodhesha takwimu hizo zilizomshangaza pia.


“Eeish, mmesema milioni 35?” Mulamwah aliuliza kwa mshangao.


Mchekeshaji huyo kutoka Magharibi mwa Kenya alitangaza kununua gari jeusi aina ya Mercedes Benz mwaka jana mwezi Machi.


“MUNGU ALIFANYA ?? mmiliki wa gari la fahari ? mercedes BENZ E250. Kila mara tembea polepole lakini sogea ipasavyo, inanipasa kumshukuru Mungu kwa baraka zote maishani. Wacha tuanzie maisha hapa. Asante kwa familia, mashabiki na marafiki kwa usaidizi wenu na maombi kila wakati,” Mulamwah alisema.

Baba huyo wa mtoto mmoja alisema kwamba sasa angalau mkewe Ruth K atakuwa anamwahisha mtoto kliniki kwa muda wakiwa ndani ya gari.


 


“Kijana wa kitale sasa ni former pedestrian. Kalamwah na mama Kalamaz sasa watakuwa wanafika kliniki kimtindo. @atruthk asante kwa support daima mamake,” alisema.


Hata hivyo, huenda madai hayo yakawa si ya kweli, kwani mwishoni mwa mwaka, mchekeshaji huyo alionyesha zaidi ya milioni moja alizokuwa amewekeza ndani ya kibubu kwa muda wa miezi 12.


Akiwaasa wenzake kuwa na mpango wa kuwekeza, Mulamwah alifichua kwamba alikuwa anawekeza kiasi cha shilingi elfu 3 kila siku kwa mwaka mzima.