MPENZI wa zamani wa Harmonize, Wolper Jackline amefichua kwamba ndoa yake na mumewe Rich Mitindo imesambaratika.
Wolper ametoa tangazo hilo kupitia kwa Instagram yake, ikiwa ni miaka miwili tu tangu walipofunga harusi yao kanisani mwishoni mwa mwaka 2022.
Wolper aliweka wazi kwamba yeye na baba wa wanawe wawili, Rich Mitindo si mtu na mumewe tena, kwani wamefikia uamuzi wa kuachana na hawahitaji ushauri wowote, haswa kuhusu kurudiana.
“Hellow Mashabiki zangu, marafiki wote mnao
nitakia mema.Ni kwa masikitiko mengi sana mmekuwa mkinitumia
message, links, na Clips mbalimbali, huku mkinishauri, kuniombea na kunitia
moyo. Nimepokea msg zenu zote kwa moyo wa Shukrani sana. Na Mungu awabariki
wote mnao nitakia mema, na hata wale wenye nia tofauti na njema pia mbarikiwe.”
“Lakini naomba niwatoe wasiwasi na mashaka juu ya
furaha na amani ya moyo wangu. Mimi na mzazi mwenzangu Rich (Baba P) hatupo
pamoja (TUMEACHANA),” Wolper alisema.
Aidha, mjasiramali huyo aliweka wazi kwamba hakuna njia yoyote ya kubadili msimamo wake kwani tayari yuko kwenye mchakato wa kuwasilisha talaka rasmi ya kutengana na Baba P, kama anavyomdekeza.
“Nipo kwenye process za Divorce/Talaka. Hivyo, mashauri yote na huruma juu ya mambo yanayo endelea na mzazi mwenzangu, msiyalete kwangu tena. Ni mtu ambae yupo huru kufanya chochote kinacho mpendeza.”
“Na hii niseme tu si kwa ubaya
haijalishi mtalipokeaje wengine lakini maisha halisi ya ndoa yangu nayajua mimi
na mwenzangu kwahiyo tutabaki kuheshimiana kama wazazi na kulea watoto wetu
lakini swala la mahusiano ya ndoa hilo halipo!
Nawapenda sana nashukuru kwa msg zenu nyingi za
kunitia moyo kutokana na mambo mnayoyaona huko lakini niwaambie tu mimi nipo
sawa na muache kunihusisha na mambo yanayoendelea kwa mzazi mwenzangu kwasababu
hayanihusu na nisingependa kuongelea hayo,” Wolper alisema.
Harusi hiyo ilizungumziwa sana mitandaoni mwezi Novemba 2022 na Wolper ambaye wengi wanamjua kama Mama P alionesha kufurahishwa kwake kupitia Instagram yake.
"Huu wakati tu?❤️❤️❤️ Moyo wa shukurani ?Wapenzi hivi karibuni tunaingia mubashara @bona_tv." Wolper alinukuu picha zilizopigwa wakati wa harusi hiyo.
Wanandoa hao walimkaribisha mtoto wao wa kwanza pamoja, mtoto wa kiume, mwaka 2021.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!