MCHUMBA wa zamani wa Enzo Fernandez amefichua jinsi nyota huyo wa Chelsea alivyomaliza uhusiano wao ghafla licha ya kuwa na watoto wawili pamoja.


Fernandez alikuwa na Valentina Cervantes tangu walipokuwa vijana, wakati kiungo huyo alipokuwa akiichezea River Plate ya Argentina, kabla ya kupata ujauzito akiwa na umri wa miaka 19 na baadaye kuhamia Benfica na Chelsea.


Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 aliigharimu Chelsea pauni milioni 107 baada ya kusajiliwa mwaka 2023 kufuatia ushindi wake wa Kombe la Dunia akiwa na Argentina.


Wawili hao walihamia katika nyumba moja huko London pamoja na binti yao Olivia na mwana wao Benjamin, wakiishi huko kwa karibu miaka miwili kabla ya Fernandez kuwasilisha habari za mshtuko kwa mpenzi wake mnamo Oktoba.


Akiongea na Game, Set & Match, Cervantes alisema: "Kila kitu kilikuwa sawa na ghafla siku moja aliniambia kuwa hataki kuwa [na mimi] tena. Kuna mambo ambayo bado natakiwa kuyashughulikia, lakini ndivyo hivyo, niliikubali."


Alisema alilia kwa dakika tano baada ya kuvunja habari hiyo na kuongeza kuwa alikataa ombi lake la kumruhusu yeye na watoto kubaki naye nyumbani - na kuishia kuhamia Argentina.


"Enzo alinipa nafasi ya kukaa kwenye nyumba ile ile tuliyokuwa tunaishi na kuniambia kuwa anaenda kupanga sehemu nyingine, lakini nilimwambia nitarudi Argentina kwa ajili ya familia yangu. Kwa sababu nilitoa kila kitu katika uhusiano huo na sijui, sijutii chochote, lakini kila kitu nilichofanya ni kwa ajili yake na kwa ajili ya familia tuliyounda."


Cervantes pia alizungumzia jinsi alivyotumia mshahara wake wote kwa Fernandez wakati wa siku za mwanzo za maisha yake ya soka alipokuwa akifanyia kazi mgahawa na kusomea shahada ya sheria.


Alisema: "Wakati huo nilipata zaidi ya [klabu] ilimpa, tulitumia mshahara wangu wote, sikuwa na chochote cha ku’save."


Alipoulizwa kama bado anampenda Fernandez, aliongeza: "Nafikiri upendo bado upo kwa sababu ni vigumu sana kuondoka haraka. Sitegemei mwanaume au mtu yeyote kuwa na furaha. Nikiwa na watoto wangu. Nitakuwa na furaha daima."


Katika mahojiano mengine na Minuto Uno, aliendelea: "Kila mtu anaichukua na kupitia michakato tofauti, nilijaribu kwenda upande wa afya. Nampenda Enzo, siwezi kumdharau. Ni mtu ambaye aliandamana nami kwa miaka mingi. nami pia nilifuatana naye, na nitaendelea kuandamana naye."