MSANII wa muziki wa Nigeria, Tiwa Savage amefunguka kuhusu talaka yake na aliyekuwa mpenzi wake Tunji ‘TeeBillz’ Balogun, na kufichua changamoto alizokumbana nazo wakati na baada ya kutengana kwao mwaka wa 2018.


Akiongea kwenye The Receipts Podcast, mwimbaji huyo alifichua kwamba mume wake wa zamani ndiye aliyehusika na mgawanyiko wao, ambao ulitokea wakati wa mapambano yake na unyogovu wa baada ya kujifungua.


Msichana huyo mwenye umri wa miaka 44 alielezea shutuma kali alizovumilia, huku Wanigeria wengi wakimgeuka na kushambulia tabia yake.


Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Alikumbuka jinsi watu mashuhuri walivyomshauri anyamaze ili kuhifadhi sifa yake, hata hali hiyo ilipozidi kumsumbua kihisia.


Tiwa alisimulia jinsi TeeBillz alitangaza maswala yao ya ndoa mtandaoni, na kumwacha kubeba mzigo wa chuki za umma.


"Nilipotoka, nilikuwa mpenzi wa Nigeria nilipoanza na sikuweza kufanya kosa lolote machoni pa Mnigeria. Nilifanya kila kitu kama ilivyotakikana. Nilienda chuo kikuu na sikuwa mama mtoto. Niliolewa kisha nikapata mtoto kwa hivyo nilifanya kila kitu kwa mpangilio sahihi na kila mtu alinipenda kisha kila kitu kilifanyika.”


“Kisha nikaanza kupata chuki kutoka kwenye blogu na nikaanza kupata chuki kutoka kwa watu fulani. Jinsi hali yetu ilivyotokea, alitangaza mtandaoni. Sikuachana naye lakini mimi ndiye nilikuwa nashambuliwa.”


Baada ya kujaribu kushiriki upande wake wa hadithi, mwimbaji alisema ukosoaji ulizidi.


“Watu walisema, ‘Unathubutu vipi kwenda kuzungumza?’ Niliambiwa singeshinda kamwe kwa sababu nilikuwa mwanamke. Ilikuwa ya kuhuzunisha moyo.”


"Wakati huo, mtoto wangu alikuwa na umri wa miezi michache tu na nilikuwa nikiugua baada ya kujifungua na mwili wangu haukuwa sawa na nilikuwa na huzuni. Kisha kila mtu alikwenda kwake na watu wachache tu walikuja kuniona.”


“Baada ya kuhojiwa ili kueleza upande wangu, hali ilizidi kuwa mbaya. Watu walikuwa kama ‘Unathubutu vipi kwenda kuzungumza’ ‘Wewe ni mwanamke na unatakiwa kujenga nyumba, ni kosa lako’.”


"Nakumbuka watu mashuhuri walinipigia simu kuniuliza jinsi ningeweza kusema upande wangu wa hadithi kwa sababu singeshinda kamwe. Tangu wakati huo, nilikuwa kama sitawahi kuzungumzia hali hiyo kwa sababu ilihuzunisha sana jinsi umma ulivyoichukulia na kunilaumu.”


 


"Ilinifungua macho na ilinifanya nishuke moyo kwa muda mrefu. Ilinikasirisha kisha nikawa ‘Msichana Mbaya wa Kiafrika.’


 


“Nilijiwazia kuwa baada ya kufanya kila kitu sawa bado nilishambuliwa. Kisha nikaanza kuchora tattoo na kuvaa sketi fupi na bikini. Nilikuwa mshamba tu,” Alisimulia mama huyo wa mtoto mmoja.