Naibu Rais Kithure Kindiki amemsifu Rais William Ruto kwa kuongoza juhudi za kuleta taifa pamoja. Kindiki alimlimbikizia sifa Ruto kwa kuwasiliana na aliyekuwa Rais Uhuru Kenyatta na aliyekuwa Waziri Mkuu Raila Odinga.

Alisema maendeleo ya nchi yatakuwa ya haraka Wakenya wote watazingatia lengo moja.

"Mnapotuongoza katika mageuzi na maendeleo ya nchi yetu, kwa wakati huu, tunawapongeza kwa kutambua kuwa maendeleo ya Kenya yatakuwa ya haraka ikiwa nchi itaungana.

Asante kwa kuwafikia wadau wengi iwezekanavyo name kuleta kila mtu mezani ili sote tuvute mwelekeo mmoja wa kuhakikisha kuwa nchi yetu inapiga hatua zaidi," Kindiki alisema.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

“Tunakupongeza kwa kuwasiliana na Waziri Mkuu wa zamani kwa ajili ya kuanzishwa kwa serikali pana, na tunakushukuru kwa kuwasiliana na aliyekuwa Rais Uhuru Kenyatta na kuhakikisha kwamba kwenda mbele sote, kila mdau mezani tunapoamua hatima ya nchi yetu na tunapoinua vizito ambavyo ni lazima tunyanyue kwa heshima ya kizazi kilichopita, na pia kwa heshima ya vizazi vijavyo.”

Kindiki aliyanena hayo wakati wa sherehe za Jamhuri Day zilizofanyika katika Bustani ya Uhuru, jijini Nairobi. Matamshi yake yanajiri wiki moja tu baada ya Rais Ruto kufanya mkutano wa faragha na Rais mstaafu Uhuru Kenyatta nyumbani kwake Ichaweri, Gatundu.

Ilikuwa ni mara ya kwanza kwa viongozi hao wawili kukutana tangu uchaguzi wa 2022. Kindiki alisema huo ulikuwa uamuzi mkubwa kwa utulivu wa nchi.

Ruto alikuwa amewasiliana na Raila mapema mwaka huu kufuatia maandamano ya Jenerali Z dhidi ya serikali na walikubali kufanya kazi pamoja.

Kufuatia makubaliano yao, angalau wanachama watano wa chama cha Raila Orange Democratic Movement (ODM) waliteuliwa katika Baraza la Mawaziri.