ALIYEKUWA rais wa chama cha wanasheria nchini, Nelson
Havi ametoa onyo kali kwa watumizi wa mitandao ya kijamii wanaotumia picha yake
kutengeneza na kueneza meme za vichekesho.
Havi alichapisha picha hiyo kwenye ukurasa wake wa X na kusema kwamba picha yenyewe tayari ameshaichukulia hatimiliki.
Picha hiyo inayomuonesha Havi amekodoa macho nje kama mtu aliyezama kwenye lindi la mawazo imekuwa ikitumika na watengeneza meme wakizua vichekesho mbalimbali.
Hata hivyo, Havi ambaye ametangaza kuwania urais mwaka 2027 na kuonyesha Imani yake ya kuwa rais wa 6 alisema kwamba yeyote atakayeitumia kuunda meme atakuwa ‘anamkosea rais wa 6 heshima’.
“Picha hii na macho ya UFO ina hakimiliki. Mtu yeyote anayeitumia katika meme atatekwa nyara na kuzuiliwa kwa siku 21. Watu wajifunze kutomdharau rais wa Sita. Uwinjo?” Havi alisema.
Hata hivyom, onyo lake lilionekana kuchochea moto wa matumizi ya picha hiyo zaidi kwenye meme za vichekesho mbaloimbali hapo hapo kwenye chapisho lake.
Havi alitangaza rasmi kuwania kiti cha urais katika uchaguzi wa 2027 baada ya miezi kadhaa ya uvumi.
Akizungumza wakati wa mahojiano ya runinga mnamo Jumatatu asubuhi Desemba 2, 2024, Havi alisisitiza hitaji la mbadala wa Rais William Ruto.
"Nitagombea urais wa Jamhuri ya Kenya mnamo 2027," alisema.
"Sasa ni dhahiri kwamba panafaa kuwa na mbadala wa Dkt. William Samoie Ruto," akaongeza.
Wakili huyo pia alimkosoa kiongozi wa upinzani Raila Odinga, akipendekeza kwamba mwelekeo wa Baba unaonekana kuelekezwa katika uongozi wa bara badala ya kuwania urais.
Havi alidai kwamba wandani wa Raila wanafanya kazi bila kuchoka ili kuchaguliwa kuwa mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika (AUC).
Licha ya kutangaza kuwania urais, Havi alisema pia yuko tayari kumpisha aliyekuwa jaji mkuu David Maraga kuwania kwa niaba yake, ikiwa jaji huyo mstaafu atakubali ofa hiyo.
“C J David Maraga ndiye mzee rahisi, wazi na mwadilifu anayehitajika kwa mabadiliko. Ikiwa atakubali, nitaacha ombi langu na kusafiri kote Kenya kumfanyia kampeni,” Havi alisema.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!