MSANII Nameless amefichua kuwa wazazi wake wanasherehekea kudumu pamoja katika ndoa kwa miongo 6.


Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Nameless alichapisha picha ya pamoja akiwa na wakongwe hao na kusema kwamba aliwatembelea nyumbani kujumuika nao wanapoadhimisha miaka 60 ya ndoa yao.


Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Msanii huyo ambaye kwa upande wake anakaribia kutimiza miaka 20 ya ndoa na mkewe Wahu Kagwi alifichua kwamba himizo na mafunzo ya ndoa ameyapata sana kutoka kwa wazee wake.


“Nilikuja nyumbani kuwaona wazazi wakisherehekea miaka 60 ya ndoa!???????? Heri ya kumbukumbu ya miaka Daddy na mama! Mifano yangu ya milele??????. Asante kwa kutuonyesha njia!️#miaka60YaUpendo&Urafiki #MyFoundation #MyLifeCoaches,” Nameless aliandika.


Mashabiki wake walimhongera kwa kufuata mfano bora wa kutoiacha ndoa kutoka kwa wazazi wake, haswa akiwa mtu maarufu.


Wahu ni miongoni mwa watu waliotuma jumbe za kuwahongera wakongwe hao kwa kushikamana kwenye ndoa katika kipindi hicho chote.


“Heri ya kumbukumbu ya miaka baba na mama!!!! ????????? Mungu aendelee kukulinda na kukuzunguka kwa wema wake!” Wahu aliandika.


Nameless na Wahu ni kati ya maceleb wachache ambao wamedumu katika ndoa kwa muda mrefu na kuwakweza kwenye nafasi iliyotukuka ya kutumiwa kama mifano bora na kioo cha jamii katika suala la ndoa na mapenzi.


Mwezi Septemba, Wahu na Nameless walisherehekea miaka 19 ya ndoa yao ambayo ilifungwa mapema miaka ya 2000s wakiwa ndio mwanzo wanajitafuta kimuziki.


Walichukua katika akaunti zao za mitandao ya kijamii kusherehekea kila mmoja kwa ujumbe ufuatao wa dhati:


 


"Leo tunasherehekea miaka 19 tangu tuseme ‘I DO!’ Kwa rafiki yangu bora, mpenzi wangu, na mshirika wangu maishani! Na tuendelee kukua na kujifunza pamoja! Heri ya kumbukumbu ya miaka, Babe! Nakupenda daima na milele ️!”


"Hapa ni kwa mengi zaidi! Na kwa familia yetu ya mtandaoni, asante kwa kutuonyesha upendo kila mara na kuwa sehemu ya safari yetu! ???? Asante, @nscbyswissbelhotel, kwa kutukaribisha kwa ajili ya kumbukumbu yetu ya mwaka.”


Wanandoa wa nguvu ya muziki walikutana kwa mara ya kwanza mnamo 1998 katika hafla ya chuo kikuu iliyofanyika kwenye uliokuwa mgahawa maarufu wa Grand Regency.


Nameless, ambaye alipenda kurap, alidokezewa kuhusu tukio hilo na rafiki yake na kuamua kutumbuiza, na kusababisha kukutana kwao kwa mara ya kwanza.