Kwa mara ya kwanza baada ya miaka mingi, timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars imeipiku Kenya kwenye msimamo wa jedwali la soka duniani, FIFA.

Tanzania ilijiimarisha kwenye jedwali  hilo baada ya kupanda juu nafasi 6 zaidi huku Kenya ikiporomoka kwa nafasi 2 chini zaidi.

Kenya ambayo awali ilikuwa katika nafasi ya 106 duniani iliporomoka hadi nafasi ya 108 huku Tanzania ikipanda kutoka nafasi ya 12 duniani hadi nafasi ya 106.

Haya yanajiri baada ya Harambee Stars kukosa kushinda mechi zao mbili zilizopita dhidi ya Zimbabwe na Namibia mtawalia.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Harambee stars


Pia walishindwa kufuzu kwa Fainali za Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025 nchini Morocco, huku Tanzania ikiifunga Guinea 1-0 na kufuzu kwa michuano hiyo ya bara Afrika.

Mnamo mwezi wa Novemba, Kenya ilisajili sare tatu - sare ya 1-1 na Namibia na Sudan Kusini (Kufuzu kwa CHAN) na sare tasa dhidi ya Zimbabwe ambayo iligonga hatma ya Kenya ya kutofunga safari yao ya AFCON kwenda Morocco mwaka ujao.

Kenya imekuwa ikifanya vibaya zaidi katika mashindano mbalimbali mwaka huu, hali ambayo imehusishwa na timu ya taifa kuchezea michuano yake mingi nje ya nchi.

FIFA na CAF walikataa kuidhijmisha viwanja vyote vya Kenya kutumika katika michuano ya kufuzu kombe la dunia na AFCON katika kile walisema kwamba viwango vya viwanja vyote vikuu vya Kenya ni duni.

Kenya ilichezea mechi zao za nyumbani kufuzu kombe la dunia nchini Malawi mapema mwaka huu huku pia wakitumia viwanja vya Uganda na Afrika Kusini kushiriki mechi za kufuzu AFCON 2025 ambayo walifeli.

Katika ukanda wa Afrika Mashariki, Uganda bado ndiyo timu iliyoorodheshwa bora kwenye nafasi ya 88 ikifuatiwa na Tanzania iliyo na 106 na Kenya 108.

Uganda na Tanzania zimefuzu kwa AFCON 2025 itakayofanyika Morocco kuanzia Jumapili, 21 Desemba 2025 hadi Jumapili, 18 Januari 2026.



Timu 5 bora duniani kwa wakati huo hazijabadilika, huku Argentina bado ikiorodheshwa kuwa timu bora zaidi Duniani. Ufaransa, Uhispania, Uingereza na Brazil wanakamata nafasi nyingine tano za juu mtawalia.