AFISA mkuu mtwendaji wa halimashauri ya hatimiliki za kazi za Sanaa humu nchini MCSK, Ezekiel Mutua ametupwa katika kipindi cha maomboleza baada ya kufiwa na baba.

Mutua alitoa taarifa hizo kupitia ukurasa wake wa Facebook ambapo alichapisha picha ya pamoja na mkongwe huyo ikionekana ni majira ya jioni.

Akimuomboleza, alisema kwamba atakachokikosa zaidi ni nyakati hizo za jioni ambapo mara kwa mara wangejumuika kwa soga humu wakiaga kutwa.

“Jioni kama hizo hazitakuwa tena, lakini katika kila kitu tunashukuru na kuthamini kumbukumbu nzuri. Nimepoteza rafiki mkubwa. Nenda salama baba. . .” Ezekiel Mutua aliandika.

Kifo cha baba kimetokea takribani miaka 2 tu baada ya mamake kufa.

Akiarifu kuhusu kifo cha rafiki yake wa karibu – mama, Mnamo Februari mwaka jana, Mutua alisema kwamba alimpoteza mmoja wa mihimili mikuu katika maisha yake.

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Baade alionekana kufululiza machapisho ya jinsi amekuwa akikaa karibu na mzee babake ili kumfariji, akisema kwamba ni Dhahiri kifo cha mamake kilimuathiri sana babake.

Katika sasisho jingine, Mutua japo kwa kumuombileza, alimsherehekea babake na kumshukuru Mungu kwa kuipa familia fursa ya kuishi naye hadi umri wa miaka 100.

Alifichua kwamba babake ni mmoja kati ya watu wachache walio hai hadi leo hii na ambao walishuhudia kutokea kwa vita vya kwanza na pili vya dunia.



“Sio wengi wanaopata fursa ya kufikisha miaka 100 na kuondoka duniani wakiwa wamezungukwa na wajukuu wao wakuu. Baba aliona Vita vya Kwanza na vya Pili vya Dunia na ameshuhudia takriban njaa na magonjwa ya mlipuko katika historia iliyorekodiwa.”

“Kuondoka kwa baba ni chungu lakini ameacha urithi wa hali ya juu,” Mutua aliongeza huku akinukuu kifungu cha Biblia kitabu cha Ayubu.

Kifo cha babake kinatokea wakati ambapo Mutua anapitia wakati mgumu katika ofisini yake baada ya baadhi ya watu waliodaiwa kuwa wanachama wa MCSK kutoa taarifa kwamba amesimamishwa kazi kama bosi wa halimashauri hiyo.

Hata hivyo, ni barua ambayo Mutua aliipuzilia mbali siku moja baadae, aliitaja kama propaganda mbaya ambayo inaendeshwa na watu aliowazuia kuingia katika afisi za MCSK bila itifaki inayofaa.