
MWIMBAJI maarufu wa Afrobeats kutoka Nigeria,
Patoranking hatimaye amezungumza baada ya kifo cha dada yake, Chioma na mumewe.
Patoranking alivunja kimya chake kupitia ukurasa wake
wa Instagram, siku chache baada ya kuwazika wawili hao ambao waliripotiwa
kufariki katika mkasa wa mlipuko wa moto nyumbani kwao
Vyabzo vya habari za burudani kutoka taifa hilo lenye
idadi kubwa ya watu barani Afrika viliripoti kuwa tukio hilo lilitokea siku
moja baada ya sherehe yao ya kuwapa nyumba.
Wenzi hao walizikwa Jumamosi, Novemba 23 2024, katika
jimbo la Ebonyi.
Walakini, akizungumza kwa mara ya kwanza baada ya
tukio hilo, Patoranking katika chapisho kwenye hadithi yake ya Instagram mnamo
Jumatatu, Novemba 25, aliandika, "mbingu pekee ndiyo inajua."
Taarifa za Patoranking kufiwa na dadake na shemeji
yake kwa wakati mmoja zilizagaa mitandaoni miezi mitatu iliyopita ambapo
shughuli za mazishi zimejikokota kwa zaidi ya siku 90.
Jirani alisimulia mlipuko huo, akisema, "Ilitokea
mtaani kwangu. Tulisikia tu mlipuko huo alasiri. Tulipokimbilia eneo la tukio,
moshi ulikuwa ukifuka kutoka kwenye jengo jipya. Vifaa vyote vya kielektroniki
viliharibiwa, na dari, milango, madirisha, na vioo viliharibiwa vibaya sana.”
Chioma Onuabuchi, dadake Patoranking aliaga dunia kwa
kutokana na majeraha yake mnamo tarehe 31 Agosti, huku mumewe George Onuabuchi akifuata
kwa huzuni Septemba 11.
Wanandoa hao waliacha nyuma mtoto wa kiume mwenye
umri wa miaka mitatu, ambaye kwa bahati nzuri alikuwa na bibi yake wakati wa
tukio hilo.
Mazishi ya Chioma na George yalifanyika Jumapili,
Novemba 24, 2024.
Ilikuwa tukio chungu kwa mwimbaji na familia yake.
Kumbuka kwamba Patoranking alisherehekea dada yake na mumewe siku ya harusi yao
mnamo 2021 na zawadi mpya ya gari.
Msanii huyo wa kibao cha Abule aliandika chapisho
lake la mwisho kwenye Instagram mnamo Agosti 20, 2024, na mashabiki walichukua
muda kwenye mitandao ya kijamii kumuhurumia yeye na familia yake.
Comments 0
Sign in to join the conversation
Sign In Create AccountNo comments yet. Be the first to share your thoughts!