MSANII mmiliki wa lebo ya Bad Nation, Marioo amefunguka sabbau ya yeye na mwenazake wa Konde Gang, Harmonize wanapenda kuimba nyimbo za mapenzi na kuumizwa kimapenzi.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kudokeza ujio wa ngoma nyingi za kolabo na Harmonize, Marioo alisema kwamba wote wawili huwa wanaendana sana katika mtiririko pindi wanapoingia kwenye studio kurekodi.

Alikiri kwamba yeye na Harmonize ni wasanii wakali ambao siku zote wakikutanisha ukali wao wa cheche, moto unakuwa wa kipekee.

“Mimi na Harmonzie, kwanza sisi wote wakali, kwa hiyo cheche zikikutana lazima zitengeneze moto mkubwa. Na ndio maana mipango yote tunapanga wakati wa kazi inafanikiwa. Huwa tunakaa, tunapanga tunatoa wimbo na pia tunasaidiana kuisukuma.”

Enjoying this article? Subscribe for unlimited access to premium sports coverage.
View Plans

Marioo alimsifia Harmonize kuwa ni msanii wa kipekee katika uandishi wa mashairi ya Kiswahili na haswa katika midundo ya Bongo Fleva.

“Sisi tunapenda kuimba hizo nyimbo. Tunapenda Bongo Fleva, tunapenda kuimba nyimbo za mapenzi na kuumizwa kwa sababu tunaziweza sana. Lakini kinachosababisha hivi vyote nafikiri ni chemistry tu. Unaeza kuta wasanii wengi ni wakali lakini kama hawana chemistry ya aina Fulani vile,” alisema.

Marioo alisisitiza kwamba heshima yake kwa Harmonize haiwezi kupimika kwa mizani ya dunia hii, akimiminia sifa kwa kufanikisha kolabo yao ya kwanza ‘Naogopa’ kuwa sauti kubwa ambayo mkapa sasa inasimika jina la wawili hao kwenye rubaa za kolabo bora za muongo katika Bongo Fleva.

Marioo alitumia mahojiano hayo kunyoosha maelezo kuhusu uvumi wa kuwepo kwa bifu kati yake na aliyekuwa mcheza densi wake, Chino Kidd.

Marioo alisema kwamba kinyume na dhana pana kuwa hawapatani, yeye na Chino na marafiki wa karibu ambao Amani imetawala kati yao.

Msanii huyo alipoulizwa kama anahisi amechangia katika maisha ya mafanikio ya Chino Kidd, alisema kwamba yeye anahisi kabisa kwamba anachomiliki ni chake kwa sababu pia anafanya kazi kwa bidii kama msanii wa Amapiano ya Kiswahili.


Chino na Marioo walipapurana kwenye mitandao ya kijamii wiki kadhaa zilizopita, Marioo akimtuhumu Chino kwa kujaribu kumtilia sumu ili kumuua.